Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNWTO yatangaza orodha ya vijiji 32 Bora vya Utalii duniani

Mlima wa Choke ni mlima wa tatu kwa urefu nchini Ethiopia, ulioko kilomita 300 kaskazini magharibi mwa mji mkuu, Addis Ababa.
Picha: WTO
Mlima wa Choke ni mlima wa tatu kwa urefu nchini Ethiopia, ulioko kilomita 300 kaskazini magharibi mwa mji mkuu, Addis Ababa.

UNWTO yatangaza orodha ya vijiji 32 Bora vya Utalii duniani

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Kutoka Austria hadi Vietnam, maeneo 32 kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni yametajwa kuwa 'Vijiji Bora vya Utalii kwa mwaka 2022' na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UNWTO).

Tuzo hiyo inatambua maeneo ya vijijini ambayo yanakumbatia utalii kama kichocheo cha maendeleo na fursa mpya za ajira na mapato, huku kikihifadhi na kukuza maadili na bidhaa za kijamii.

Katibu Mkuu wa UNWTO Zurab Pololikashvili amesema “Kwa jamii za vijijini kila mahali, utalii unaweza kuwa jambo la kuleta mabadiliko ya kweli katika kutoa ajira, kusaidia biashara za ndani na kudumisha uhai wa mila. Vijiji Bora vya Utalii na UNWTO vinaonyesha uwezo wa sekta ya kuendeleza mseto wa kiuchumi na kuunda fursa kwa wote nje ya miji mikubwa.”

Watalii na wenyeji wakiwa na furaha pamoja katika milima ya Choke nchini Ethipia
Picha: WTO
Watalii na wenyeji wakiwa na furaha pamoja katika milima ya Choke nchini Ethipia

Mpango huu wa utambuzi wa vijiji wa UNWTO unatambua vijiji kwa kujitolea kwao katika uvumbuzi na uendelevu katika nyanja zake zote za kiuchumi, kijamii na kimazingira pamoja na kuzingatia kuendeleza utalii kwa kuzingatia Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Kwa mwaka huu wa 2022, jumla ya vijiji 32 kutoka nchi 18 katika kanda tano za ulimwengu vilipewa tuzo hiyo. Vijiji hivi vilifanyiwa tathmini na Bodi huru ya ushauri kwa kuzingatia vigezo vinavyojumuisha maeneo tisa ambavyo ni:

  1. Utamaduni na Maliasili
  2. Ukuzaji na Uhifadhi wa Rasilimali za Utamaduni
  3. Uendelevu wa Kiuchumi
  4. Uendelevu wa Kijamii
  5. Uendelevu wa Mazingira
  6. Maendeleo ya Utalii yaliyounganishwa na mnyororo wa thamani
  7. Utawala ulioweka kipaumbele kwenye Utalii
  8. Miundombinu iliyounganishwa
  9. Afya, Usalama na Ulinzi.
Kutoka Austria hadi Vietnam, maeneo 32 kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni yametajwa kuwa 'Vijiji Bora vya Utalii kwa mwaka 2022
© UNWTO
Kutoka Austria hadi Vietnam, maeneo 32 kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni yametajwa kuwa 'Vijiji Bora vya Utalii kwa mwaka 2022

Katika toleo la mwaka huu jumla ya vijiji 136 vilipendekezwa kutoka nchi 57 wanachama wa UNWTO. Kila nchi mwanachama inaweza kuteua vijiji vitatu. Kutoka katika orodha hiyo 32 vilitambuliwa kama Vijiji Bora vya Utalii na UNWTO. Vijiji hivyo ni

  1. Zell am See, Austria
  2. Wagrain, Austria
  3. Puqueldón, Chile
  4. Dazhai, China
  5. Jingzhu, China
  6. Choachí, Colombia
  7. Aguarico, Ecuador
  8. Angochagua, Ecuador
  9. Choke Mountains Ecovillage, Ethiopia
  10. Mestia, Georgia
  11. Kfar Kama, Israel
  12. Sauris-Zahre, Italia
  13. Isola del Giglio, Italia
  14. Umm Qais, Jordan
  15. Creel, Mexico
  16. El Fuerte, Mexico
  17. Ksar Elkhorbat, Morocco
  18. Moulay Bouzerktoune, Morocco
  19. Lamas, Peru
  20. Raqchi, Peru
  21. Castelo Novo, Ureno
  22. Pyeongsa-ri, Korea Kusini
  23. Rasinari, Romania
  24. AlUla Old Town, Saudi Arabia
  25. Bohinj, Slovenia
  26. Rupit, Hispania
  27. Alquézar, Hispania
  28. Guadalupe, Hispania
  29. Murten, Uswisi
  30. Andermatt, Uswisi
  31. Birgi, Türkiye
  32. Thái Hải, Vietnam
Milima ya Choke ilioko nchini Ethiopia imetambuliwa na WTO kuwa kati ya vijiji Bora vya Utalii 2022.
Picha: WTO
Milima ya Choke ilioko nchini Ethiopia imetambuliwa na WTO kuwa kati ya vijiji Bora vya Utalii 2022.

Mbali na kutangazwa kwa vijijini 32 bora, vijiji vingine 20 vitaingia kwenye program ya maboresho.

Vijiji vyote 52 pia vitakuwa sehemu ya mtandao Bora wa Kimataifa wa Vijiji vya Utalii wa UNWTO ulioundwa mwaka 2021 ambao umelenga kukusanya vijiji 115 kutoka mabara matano.

Mtandao huo unamanufaa kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwapatia mafunzo  ana kwa ana na kw anjia ya mtandao, vijiji hivyo vitaweza kushirikishana uzoefu wa yale yanayofanya kazi vizuri katika maeneo mbalimbali pamoja na utambuzi wa chapa ya kimataifa na uhamasishaji.

Vijiji hivyo 20 ni

  1. Trevelin, Argentina
  2. Krupa na Vrbasu, Bosnia-Herzegovina
  3. Fontainhas, Cabo Verde
  4. Ninhue, Chile
  5. San Vicente de Chucuri, Colombia
  6. Barichara, Colombia
  7. Kalopanagiotis, Cyprus
  8. Pissouri, Cyprus
  9. Adaba, Ethiopia
  10. Khonoma, India
  11. Neot Semadar, Israel
  12. Otricoli, Italy
  13. Il Ngwesi, Kenya
  14. Grand Baie, Mauritius
  15. Bella Vista, Paraguay
  16. Istebna, Poland
  17. Ferraria de São João, Portugal
  18. Castara, Trinidad and Tobago
  19. Anıtlı, Türkiye
  20. Cumalıkızık, Türkiye
Utalii endelevu unafaida kwa mazingira, uchumi na kwa jamii
© UNWTO
Utalii endelevu unafaida kwa mazingira, uchumi na kwa jamii

Utalii kama kichocheo cha maendeleo vijijini na ushirikishwaji

Mpango wa Vijiji Bora vya Utalii ni mradi mkuu wa Mpango wa Maendeleo ya Utalii wa UNWTO kwa Maendeleo Vijijini.

Mpango huu unalenga kuhakikisha utalii unachangia katika kupunguza ukosefu wa usawa wa kikanda katika mapato na maendeleo, kupambana katika kupungua idadi ya watu wanao ondoka vijijini, kuendeleza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na vijana, kuendeleza ubunifu na digitali, kuboresha mawasiliano, miundombinu, upatikanaji wa fedha na uwekezaji, ubunifu katika maendeleo ya bidhaa na thamani, kuongeza mnyororo wa thamani, kukuza mazoea endelevu ya matumizi bora ya rasilimali na kupunguza uzalishaji na upotevu na kuimarisha elimu na ujuzi.

Mpango huu unalenga kukuza utawala bora wenye ushirikiano wa ngazi mbalimbali na unaowashirikisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha wanajamii.