Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Kumbukumbu ya mishumaa kwa wale waliopoteza maisha kwa VVU na UKIMWI, Yerevan, Armenia.
Photo IOM Armenia 2018
Kumbukumbu ya mishumaa kwa wale waliopoteza maisha kwa VVU na UKIMWI, Yerevan, Armenia.

Nchi wanachama zaanza kuongeza ufadhili UNAIDS

23 Juni 2022
Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na UKIMWI, UNAIDS limeshukuru mataifa yaliyoanza kuongeza fedha za ufadhili kwa ajili ya shughuli za uwekezaji ili kumaliza UKIMWI duniani.

Taarifa iliyotolewa na UNAIDS kwa waandishi wa Habari kutoka Geneva Uswisi imemnukuu Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Winnie Byanyima akieeleza shida kubwa walizokumbana nazo wakati ufadhili ulipokuwa mdogo na kueleza ufadhili wenye nguvu na unaotabirika ni muhimu kwa kuokoa Maisha na kumaliza janga la UKIMWI.

“Ni gharama zaidi kutokomeza janga la UKIMWI kuliko kumaliza UKIMWI wenyewe, mamia ya maelfu ya vifo na mamilioni ya maambukizi mapya yote yanaweza kumalizika.” Alisema Byanyima

Nchi zilizotangaza kuongeza ufadhili ni Uingereza na Ujerumani. Uingereza imetangaza ufadhili wake kwa mwaka huu kwa UNAIDS dola milioni 9.8 ikiwa ni ongezekoa la zaidi ya dola milioni 3 ikilinganishwa na mwaka 2021.

Ujerumani nayo imetangaza itafadhili UNAIDS na dola milioni 7.3 ikilinganishwa na dola milioni 6.1 walizofadhili mwaka jana ikiwa ni njia moja wapo ya kuipongeza UNAIDS kwa kazi nzuri ya kusaidia wagonjwa wenye Virusi Vya UKIMWI VVU pamoja na huduma nyingine za afya hususan katika maenep yenye migogoro duniani kote ikiwa ni pamoja na Ukraine n anchi jirani.

Akizungumza katika maandalizi ya mkutano wa saba wa nchi wanachama Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa ufadhili Peter Sands amesema “ili kuwezesha mfuko wa ufadhili wa kimataifa kutimiza malengo yake tunahitaji kuongeza fecha na tunahitaji UNAIDS iwe imefadhiliwa kikamilifu. Hatuwezi kufanya hivyo bila kuwa na fecha na hatuwezi kufanya mazingaombwe ili kuwa na matokeo bora bila kuongeza rasilimali.”

Nchi ya Kenya ikiwakilisha kundi la nchi za Afrika katika mkutano huo ilisema nchi zote ulimwenguni zinategemea UNAIDS ili ziweze kufikia mwisho wa UKIMWI. 

UNAIDS ni Mpango pekee wa pamoja wa Umoja wa Mataifa, wa kipekee unaoleta pamoja mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo ni UNICEF, UNESCO, UN Women, UNHCR, WFP, UNDP, UNFPA, UNODC, ILO, Benki ya Dunia na WHO ili kwa pamoja UNAIDS inachanganya aina mbalimbali za utaalamu wa kiufundi, na kazi za sekta mbalimbali ili kuweza kumaliza janga la UKIMWI.

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
UKIMWI|ufadhili

Taarifa Zihusianazo

WFP imelazimika kupunguza mgao wa chakula Sudan Kusini na baadhi ya sehemu za  Afrika Mashariki

Ukata wazidisha ongezeko la njaa miongoni mwa wakimbizi:WFP 

Mwanamume akipokea dawa za matibabu dhidi ya VVU wakati wa janga la COVID-19 nchini Colombia.

Ushirikiano ni muhimu kutokomeza UKIMWI ifikapo 2030 

wakimbizi wa Kisomali katika kambi ya Daadab, Kenya.

Wakimbizi ndio wanaobeba gharama kubwa kwa kukosa ufadhili:UNHCR

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials