Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

UNESCO inasema kauli za chuki zinaongezeka duniani kote
Unsplash/Jon Tyson
UNESCO inasema kauli za chuki zinaongezeka duniani kote

Kauli za chuki ni hatari kwa kila mtu: Guterres

18 Juni 2022
Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema kauli za chuki ni hatari kwa watu wote na kila mtu anao wajibu wakuzuia kauli hizo katika jamii.

Katika taarifa yake iliyotolewa kwa waandishi wa habari hii leo jijini New York, Marekani ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga kauli za chuki duniani amesema “Wote tuweke ahadi ya kutumia uwezo wetu wote kumaliza kauli za chuki kwa kuhamasisha kuenzi tofauti zetu na kujumuisha kila mtu”

Mwaka jana (2021), Baraza Kuu LA Umoja wa Mataifa lilikutana ili kupitisha azimio la kutaka kuwepo na mazungumzo kuhusu tamaduni na dini mbalimbali ili kukabiliana na kauli za chuki pamoja na kutangaza Siku ya Kimataifa ambayo kwa mara ya kwanza inaadhimisha leo.
Ukuaji wa mitandao ya kijamii unaelezwa kuwa moja ya visababishi vikubwa vinavyoeneza kauli za chuki, wakati wa janga la COVID-19 kulienea kauli za chuki dhidi ya watu wachache na hii kuthibitisha kuwa jamii nyingi ziko hatarini kwa unyanyapaa, unaguzi na mambo mengine yanayoendana na hayo.
Guterres anasema ili kukabiliana na tishio hilo ndio maana “miaka mitatu iliyopita, nilizindua Mkakati na Mpango wa Utekelezaji wa Umoja wa Mataifa kuhusu kauli za chuki. Hii inatoa mfumo wa msaada wetu kwa Nchi Wanachama kukabiliana na janga hili huku zikiheshimu uhuru wa kujieleza na kutoa maoni, kwa ushirikiano na mashirika ya kiraia, vyombo vya habari, makampuni ya teknolojia na majukwaa ya mitandao ya kijamii.”

Hatari ya kauli za chuki

Kauli za chuki zina chochea vurugu, hudhoofisha utofauti ndani ya jamii, na kutishia maadili na kanuni zinazo unganisha jamii kwa pamoja.

Maneno haya yanapotumika yanaweza kuwa ni silaha na kusababisha madhara ya kimwili. Kuongezeka kutoka kwa matamshi ya chuki hadi ghasia kumechangia pakubwa katika uhalifu wa kutisha wa zama za kisasa, kutoka chuki dhidi ya Wayahudi inayoendesha mauaji ya Holocaust, hadi mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda.

Kauli hizi zinapotumika zinakuza ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni, chuki dhidi ya wanawake, kudhalilisha watu binafsi na jamii, na ina athari kubwa kwa juhudi za kukuza amani na usalama, haki za binadamu na maendeleo endelevu SGDs.

 

♦ Kurambaza ukurasa mahsusi wa Siku ya Kiswahili Duniani bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Siku za UN|mauaji ya kimbari|Kauli za chuki|kauli za chuki mtandaoni|António Guterres|Holocaust

Taarifa Zihusianazo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres

Kuruhusu kauli za chuki ni kushambulia moja kwa moja maadili yetu:UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, (kulia) wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari leo Januari 18, 2019 kwenye makao makuu ya UN jijini New York

Guterres asema hofu imegeuzwa mtaji, ataja mambo 3 kutatua hali ya sasa

Picha katika makumbusho ya maangamizi makuu Marekani.

Licha ya jinamizi lake mauaji ya Holocust hayakumaliza chuki dhidi ya Wayahudi  

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials