Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Anuwai za kibayolojia kote ulimwenguni ziko hatarini kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
© Unsplash/Zdeněk Macháček
Anuwai za kibayolojia kote ulimwenguni ziko hatarini kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Tuhusishe kila mtu kuokoa anuwai za kibailojia: Guterres

22 Mei 2022
Tabianchi na mazingira

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ili dunia kufikia mustakabali endelevu kwa wote,inahitaji kuchukua hatua za haraka za kulinda bioanuwai.Guterres amesema hayo katika taarifa yake ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya utofauti wa anuwai za kibaiolojia na kusisitiza kuwa “ni lazima tukomeshe vita vyetu visivyo na maana vya uharibifu dhidi ya asili.”

Ameeleza katika taarifa yake kuwa Kiwango cha vita ya uharibifu wa asili ni kubwa kwa makumi na mamia tofauti na miaka 10 iliyopita na hali ya uharibifu inaendelea kwa kasi.
Guterres ametoa wito kwa watu wote duniani kuchukua hatua za hataka kujenga mustakabali wa pamoja kwa manufaa ya maisha ya wote ili kuokoa utajiri wa asili wa lazima na dhaifu wa sayari yetu, kila mtu anahitaji kujumuika kushughulikia changamoto hizo ikiwa ni pamoja na vijana na watu wanaoishi katika mazingira magumu ambao wanategemea zaidi asili kwa ajili ya maisha yao. 
Amekumbusha kuwa “Bioanuwai ni muhimu tunapotaka kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu, kukomesha tishio lililopo la mabadiliko ya tabianchi, kusitisha uharibifu wa ardhi, kujenga usalama wa chakula na kusaidia maendeleo katika afya ya binadamu na viumbe hai hutoa ufumbuzi tayari kwa ukuaji wa kijani na jumuishi.”

Serikali zina jukumu kubwa

Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa mwaka huu serikali zitakutana ili kukubaliana juu ya mfumo wa bioanuwai wa kimataifa wa baada ya mwaka 2020, wenye shabaha zilizo wazi na zinazoweza kupimika na njia thabiti za utekelezaji ambazo zinaweza kurejesha bayoanuwai ifikapo mwaka 2030.
“Mfumo huo lazima ushughulikie vichochezi vya upotevu wa bayoanuwai na kuwezesha mabadiliko kabambe na yakimageuzi yanayohitajika ili kuishi kwa amani na asili kwa kulinda kwa ufanisi zaidi ardhi ya dunia, maji safi na bahari, kuhimiza matumizi na uzalishaji endelevu, kutumia ufumbuzi wa asili kushughulikia hali ya hewa, kubadilisha na kukomesha ruzuku zenye madhara zinazoharibu mazingira. 
Guterres ameongeza kuwa inapaswa kuhamasisha hatua na rasilimali za kifedha ili kuendesha uwekezaji halisi wa asili, kuhakikisha kwamba sote tunanufaika kutokana na faida za bioanuwai.
“Tunapotimiza malengo haya na kutekeleza Dira ya 2050 ya "kuishi kwa upatano na asili", lazima tuchukue hatua kwa kuheshimu usawa na haki za binadamu, hasa kuhusiana na wakazi wengi wa kiasili ambao maeneo yao yana anuwai nyingi za kibaiolojia.”

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Siku za UN|António Guterres|Siku ya utofauti wa kibaiolojia

Taarifa Zihusianazo

Tangazo nje ya hospitali katika mji mkuu Monrovia,Liberia, ikiwahimiza wagonjwa wasitoe hela kwa madaktari kwa huduma yoyote.

Katu tusikubali ufisadi ukwamishe SDGs- Guterres

Sehemu ya mji wa Nairobi ambako kutokana na uchafuzi wa hali ya hewa unaosababishwa na Matatu, watu wanaweza kuathiriwa afya zao.

Kila mtu achukue hatua ili sote tuweze kuvuta hewa safi- Guterres

Watoto wa shule wakipata mlo shuleni uliopikwa kwa mboga mboga mbazo kutokana na umbo lake hakifuaa soko ya nje

Tuwekeze ili kila mtu popote alipo apate chakula bora- Guterres 

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials