Tuwekeze kwenye tafiti na matibabu ya TB kunusuru kizazi cha sasa na kijacho - WHO
Tuwekeze kwenye tafiti na matibabu ya TB kunusuru kizazi cha sasa na kijacho - WHO
WHO inasema kuwa ugonjwa wa Kifua Kikuu au TB, ulishughulikiwa ipasavyo duniani kote na kwamba maisha ya watu milioni 66 yaliokolewa.
Lakini janga la COVID-19 limebadilisha mafanikio hayo kwa kuwa rasilimali nyingi ziliwekezwa katika kupambana na janga hilo na kwa mara ya kwanza katika kipindi cha muongo mmoja, vifo vya TB viliongezeka mwaka wa 2020.
Wito wa Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dkt. Tedros Ghebreyesus katika siku hii ya TB duniani ni kwa nchi na wafadhili kuongeza matumizi katika uchunguzi, matibabu na kinga ya TB akitolea mfano mwaka 2020, ufadhili ulikuwa chini ya nusu ya lengo la kimataifa la dola bilioni 13 kila mwaka ifikapo 2022.
Leo ni Siku ya #Kifuakikuu duniani #WorldTuberculosisDay tunakupeleka nchini #Ethiopia mwaka 1964 kampeni ya chanjo ya #BCG ya kukinga Kifua Kikuu. Kampeni iliendeshwa na @WHO kwa kushirikiana na @UNICEF #tbt 📸: UN 10/Januari/1964 pic.twitter.com/RyOmqYxSLW
HabarizaUN
Dkt.Tedros amesema “uwekezaji wa haraka unahitajika ili kukuza na kupanua ufikiaji wa huduma na zana za ubunifu zaidi za kuzuia, kugundua na kutibu TB ambayo inaweza kuokoa mamilioni ya maisha kila mwaka, ukosefu wa usawa na kuepusha hasara kubwa za kiuchumi.”
Ufadhili wahitajika zaidi
Kwa upande wake Mkurugenzi wa WHO anayehusika na mipango ya kifua kikuu Dkt. Tereza Kasaeva amesema ili kunusuru kizazi cha sasa na kijacho ni vyema suala la ufadhili likashughulikuwa kwa haraka na WHO imetoa miongozo mipya ya namna ya kuwasaidaia.
Anasema watoto na vijana walio na TB wako nyuma kuliko watu wazima katika kupata kinga na matibabu, miongozo ya WHO iliyotolewa leo ni mabadiliko kwa watoto na vijana ili kuwasaidia kugunduliwa na kupata huduma mapema, na kusababisha matokeo bora na kupunguza maambukizi. Kipaumbele sasa ni kupanua haraka utekelezaji wa mwongozo katika nchi nzote iili kuokoa maisha ya vijana na kuepusha mateso.
Akinukuu ripoti ya mwaka 2020 ya TB Dkt. Kasaeva amesema, imekaridia asilimia 63 ya watoto na vijana chini ya miaka 15 wenye Kifua Kikuu hawakufikiwa na matibabu ya kuokoa maisha yao au taarifa zao hazijawasilishwa na kwa upande wa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano hali ni mbaya zaidi kwa kuwa asilimia 72 hawajafikiwa na matibabu.
WHO imeeleza takriban theluthi mbili ya watoto walio na umri wa chini ya miaka 5 waliohitimu hawakupata kinga ya kuzuia TB na hivyo kundi hilo lipo katika hatari ya kupata ugonjwa huo.