Tunaushukuru Umoja wa Mataifa na Jeshi la Tanzania kwa kuzingatia usawa wa kijinsia
Tunaushukuru Umoja wa Mataifa na Jeshi la Tanzania kwa kuzingatia usawa wa kijinsia
Tukiwa bado tuko katika mwezi wa wanawake ambao umekuwa na matukio kadhaa makubwa kama maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake duniani na siku ya majaji wanawake, wanawake wanajeshi walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu katika kikosi cha 5 kutoka Tanzania kinacholinda amani kupitia mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCAR, wameushukuru Umoja wa Mataifa pamoja na Jeshi lao la Tanzania kwa kuzingatia usawa wa kijinsia katika mipango ya ulinzi wa amani.
Mwingine ni Staff Sajenti Martha Cosmas Julius, yeye analenga kuitumia nafasi hii kubadilisha fikira za jamii kwa kuanzia na wanawake wenyewe ili lengo namba 5 la Malengo ya Maendeleo Endelevu kuhusu Usawa wa Kijinsia litimie huku akitoa ahadi kwamba kwa nafasi yake kama mlinda amani mwanamke, atajitahidi sana kuwaelimisha wanawake wenzake, "kwamba mwanamke anaweza kupata au kusababisha maendeleo yakapatikana. Kinachotakiwa ni kwamba hatakiwi mwanamke au wanawake hatutakiwi kuangalia ni changamoto gani ambazo zinajitokeza au tunazozipitia kikubwa ni kusonga mbele kwa lengo la kupata maendeleo au kufanikisha maendeleo katika jamii na ninachoamini ni kwamba penye mafanikio au penye maendeleo pana sauti na nguvu kubwa ya mwanamke.”