Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usinyanyapae watu wenye umri mkubwa kwenye Akili bandia

Uhandisi unaweza kuchukua jukumu muhimu katika kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu.
Unsplash/Possessed Photography
Uhandisi unaweza kuchukua jukumu muhimu katika kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Usinyanyapae watu wenye umri mkubwa kwenye Akili bandia

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Sera mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO kuhusu ubaguzi wa uzee katika mifumo ya akili bandia iliyoandaliwa kwa ajili ya huduma za afya, inawasilisha hatua za kisheria, zisizo za kisheria na za kiufundi ambazo zinaweza kutumika kupunguza hatari ya kuzidisha au kuanzisha ubaguzi wa umri mkubwa au uzee  kupitia teknolojia hizi. 

 

Teknolojia za akili Bandia (AI) zinaleta mapinduzi katika nyanja nyingi ikijumuisha afya ya umma na dawa kwa wazee ambapo zinaweza kusaidia kutabiri hatari na matukio ya kiafya, kuwezesha ukuzaji wa dawa na mengine mengi lakini kuna wasiwasi  kwamba ikiwa hazitadhibitiwa, teknolojia za akili bandia zinaweza kuendeleza ubaguzi wa uzee uliopo katika jamii na kudhoofisha ubora wa afya na huduma za kijamii ambazo wazee hupokea. 

Teknolojia za akili Bandia (AI) zinaweza kuboresha afya na ustawi wa watu wazee, lakini tu iwapo ubaguzi wa umri mkubwa au uzee utaondolewa kwenye muundo, utekelezaji na matumizi yao.