Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Kambini Dadaab
UNHCR
Kambini Dadaab

Marekani yatoa msaada wa taulo za kike kusaidia elimu kwa wasichana Dadaab:UNHCR

29 Novemba 2021
Msaada wa Kibinadamu

Mano Hamdam mwenye umri wa miaka 20 anakumbuka machache sana kuhusu maisha aliyokuwa akiishi huko Kismayo nchini Somalia.  

Baba yake alifariki dunia mwaka 2006 na familia ilikabiliwa na changamoto kubwa ya fedha huku mama yake akijaribu kupata rizki kwa kila njia. 

Kifo cha baba yake ambaye alikuwa ndio tegemeo kuu la familia pamoja na ukosefu wa usalama nchini Somalia viliilazimisha familia hiyo ya watu wanane kufungasha virago na kukimbilia nchi Jirani ya Kenya mwaka 2006. 

Akikua, Mano na dada zake wanne hawakuwa na uwezo wa kununua au kupata taulo za kike na hawakuwa na jinsi bali kutafuta njia mbadala. “Tulirarua nguo zetu vipande vipande na kuvitumia kama taulo za kike.

Tangu mwaka 2020 shirika la kiraia la Hope in the Street nchini Kenya limekuwa likiwapatia wakazi wa mitaa ya mabanda jijini Nairobi misaada muhimu kama vile sodo au taulo za kike, viatu, chakula na mengineyo muhimu.
UN/ Jason Nyakundi
Tangu mwaka 2020 shirika la kiraia la Hope in the Street nchini Kenya limekuwa likiwapatia wakazi wa mitaa ya mabanda jijini Nairobi misaada muhimu kama vile sodo au taulo za kike, viatu, chakula na mengineyo muhimu.

Kama hatukuwa na smut aliyetusitiri na taulo za kike basi kutumia vipande tulivyochana chana vya nguo zetu ndio ilikuwa suluhu.” 
Ukosefu wa taulo za kike kwa wasichana kambini Dadaab mara nyingi husababisha wasichana wa shule  kukosa khudhuria masomo kila mwezi wanapokuwa hedhini. 
Nino Omar mwenye umri wa miaka 19, anasoma darasa moja na Mano aliye na ndoto ya kuwa profesa wa masuala ya tiba.  

Nino anasema taulo za kike wanazopewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR  na wadau wengine hazitoshi. “Kutokana na ukosefu wa nafasi za kazi, familia haziwezi kumudu kununua taulo za kike, Kwa wasichana wengi hata hawana uhaka na kile wanachopaswa kufanya wakati wakiwa kwenye siku zao,” anaongeza. 

Kambi ya Dadaab nchini Kenya, ni moja ya kambi kubwa zaidi za wakimbizi duniani.
IOM/UNHCR/Brendan Bannon
Kambi ya Dadaab nchini Kenya, ni moja ya kambi kubwa zaidi za wakimbizi duniani.

Kwa mujibu wa Martha Kow-Donkor, afisa wa UNHCR kwenye kambi ya Dadaa, tamaduni na dini pia huwa kizuizi kwa elimu kuhusu afya ya wasichana kwa kuwa elimu kama hiyo haitolewi nyumbani. “Wasichana hutegema marafiki kupata habari ambayo inaweza kuwa imepotoshwa. Kwa hivyo kuna hitaji la elimu ya hali ya juu ya afya na ngono kwa wasicna hawa n ani elimu iliyo sahihi shuleni” 

Binti akiwa ameshikilia vitabu msaada wa Umoja wa Ulaya kwa watoto wakimbizi katika kambi ya Dadaab nchini Kenya
© UNHCR/Mohamed Aden Maalim
Binti akiwa ameshikilia vitabu msaada wa Umoja wa Ulaya kwa watoto wakimbizi katika kambi ya Dadaab nchini Kenya

Changamoto hizi zinazowakumba wanafunzi wasichana hazidhuru tu matokeo yao shuleni lakini pia huwapokonya heshima, kujithamini na kujiamini kwao.  
Hofu yao kubwa ni kujichafua hali ambayo husababisha kejeli kutoka kwa wanafunzi wa kiume shuleni. 
  
“Kuepuka hili, wasichana huchagua kukosa masomo wakati wa hedhi. 
Baadhi ya wasichana huchagua kulala darasani, na baadhi huomba ruhusa kwenda msalani mara kwa mara na kupoteza muda muhimu wa masomo,” anasema afisa huyo wa UNHCR. 
Mwezi Agosti mwaka huu 2021 shirika la UNHCR kwenye kambi ya Dadaab lilipokea msaada wa taulo za kike 100,000 ili ziweze kusambazwa kwa wasichana wakimbizi katika shule zote za msingi na upili katika kambi ya Dadaab. 
  
Kutokana na usaidizi huo kutoka kwa wafadhili kama vile serikali ya Marekani ambayo mara kwa mara imetoa bidhaa hizo, sasa wasichana wengi wameanza kuhudhuria masomo kikamilifu. 
  
Mano aliye na matumaini kila wakati, ana ndoto ya kuwa daktari na kuishi na kurejea familia yake nchini Somalia. 
  
“Mara nitakapokamilisha masomo yangu, ninataka kurejea Somalia na kuwaelimisha wasichana kuhusu usafi na ikiwezekena nitengeneze taulo za kike kwa wasichana wote nchini Somalia,” anasema Mano. 
TAGS: UNHCR, Dadaab, Somalia, wasichana, taulo za kike, elimu 
 

 

♦ Kurambaza ukurasa mahsusi wa Siku ya Kiswahili Duniani bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
wasichana|taulo za kike|elimu

Taarifa Zihusianazo

Janga la Corona limeathiri namna watu wanapitia hedhi salama.

Wanawake na wasichana wakimbizi wahaha kupata taulo za kike DRC, UNHCR yawasaidia 

Angelique Kidjo ambaye ndiye muasisi wa wakifu wa Batonga akitoa maelfu ya viatu kwa wasichana nchini Benini.

Viatu ni sehemu ya kumchagiza mtoto kwenda shule-Kidjo 

Binti akiwa ameshikilia vitabu msaada wa Umoja wa Ulaya kwa watoto wakimbizi katika kambi ya Dadaab nchini Kenya

Programu ya UNICEF nchini kenya yawasaidia watoto wa kike kurejea shuleni

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials