Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Mama Mjane anayelea wajukuu wake watatu huko Douala, Cameroon.
UN Women/Ryan Brown
Mama Mjane anayelea wajukuu wake watatu huko Douala, Cameroon.

Katika wakati huu mgumu wa COVID-19 tusiwape kisogo wajane:Guterres

23 Juni 2021
Msaada wa Kibinadamu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameiasa dunia kutowasahau wajane hasa wakati huu wa janga la corona au COVID-19 ambapo wanaume wengi wanaendelea kupoteza maisha na kuwaacha wake zao wakihaha na familia. 

Kupitia ujumbe wake wa siku ya wajane duniani inayoadhimishwa leo Juni 23 Antonio Guterres amesema “Huu ni wakati muafaka wa kuzingatia mwelekeo wa mara kwa mara uliosahaulika wa shida, maisha na hatima ya wajane walioachwa nyuma. Kifo cha mwenzi wakati wowote kinaweza kuwaacha wanawake wengi bila haki ya urithi au mali. Wakati wa janga hasara hizi mara nyingi huongezeka kwa wajane na huambatana na unyanyapaa na ubaguzi.” 

Guterres ameongeza kuwa viwango ambavyo havijawahi kutokea vya kutengwa na changamoto za kiuchumi zilizoletwa na mgogoro wa COVID-19 zinaweza kudhoofisha zaidi uwezo wa wajane wa kujikimu na familia zao, na kuwaternganisha na uhusiano wa kijamii wakati ambao ni wa huzuni kubwa. 
Katibu Mkuu amesisitiza kuwa “Tunapojitahidi kushughulikia COVID-19, serikali lazima zifanye kazi kujumuisha msaada kwa mahitaji ya haraka ya wajane katika mipango ya kichocheo cha fedha, kwa mfano kupitia ufikiaji wa uhamishaji wa kuchangisha pesa.“

Mbali ya hayo amesema dunia inapojitahidi kujikwamua kutoka kwenye janga hili juhudi hizo lazima zifuatwe na mabadiliko ya kimuundo ya muda mrefu, pamoja na kumaliza sheria za kibaguzi zinazowanyima wanawake haki sawa na wanaume na kuhakikisha upatikanaji wa ulinzi wa jamii, ili wanawake wasianze kwa hasara.  
Pia ameongeza kuwa “Tunahitaji takwimu bora, zilizogawanywa kwa minajili ya umri na jinsia, kuhakikisha kuwa wajane wanahesabiwa na kuungwa mkono, sasa na katika siku zijazo.” 

Katika siku hii ya wajane Guterres amehimiza kuwa “Hebu tuimarishe jamii zetu, tahamani ya familia na kuzijenga upya jamii ambazo zinawaunga mkono na kuwasaidia wajane katika kila nyanja.” 
 
 

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Siku za UN|Siku ya wajane|COVID-19

Taarifa Zihusianazo

Wahudumu wa afya wakitoa matibabu kwa mtoto wa umri wa miaka 15 ambaye anashukiwa kuugua Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC.

Wahudumu wa kibinadamu ni wa kwanza kuwasIli na wa mwisho kuondoka kwenye kila janga- Profesa Tijjani-Bande

Marie-Noelle mwenye miaka 22, mjane mwenye watoto watatu na manusura wa ukatili wa kingono DRC, ni mmoja wa wanajumuiya wa umoja wa kina mama wa Mokolo kikundi kinachowasaidia wanawake na kuwawezesha.

Lazima tuhakikishw wajane hawaachwi nyuma:UN

Mnamo tarehe 30 Machi, León mwenye umri wa miezi 7 na wazazi wake wakitazama maonyesho ya kila siku ya bandia yaliyowekwa na majirani zao wakati huu wa COVID-19 ili kuburudisha mtoto.

Msaada wahitajika kwa wazazi wakati COVID-19 ikiendelea:UN

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials