Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Jirani ya Delmas 32 katika mji mkuu wa Haiti, Port au Prince ni moja ya mahali ambapo kuna umasikini zaidi katika nchi za Karibea
World Bank/Dominic Chavez
Jirani ya Delmas 32 katika mji mkuu wa Haiti, Port au Prince ni moja ya mahali ambapo kuna umasikini zaidi katika nchi za Karibea

Haiti: Ukosefu wa fedha unaweka rehani maisha ya watoto 86,000

31 Mei 2021
Msaada wa Kibinadamu

Idadi ya Watoto chini ya miaka 5 wanaougua utapiamlo mkali nchini Haiti inaweza kuongezeka zaidi ya mara mbili mwaka huu, ameonya Jean Gough mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto – UNICEF katika ukanda wa Amerika kusini na karibiani, wakati akihitimisha ziara yake ya siku 7 katika nchi hiyo. 

Zaidi ya Watoto 86,000 nchini Haiti walio chini ya umri wa miaka 5 wanatabiriwa kupata utapiamlo mkali mwaka huu, ikilinganishwa na Watoto 41,000 mwaka jana, na wanaweza kupoteza maisha iwapo hawatapata msaada wa haraka. 

UNICEF imeshitushwa na ongezeko hilo la utapiamlo katika kipindi cha mwaka mmoja na imeonesha wasiwasi wake kutokana na upungufu wa chakula kilichotayari kama matibabu kwa wiki zijazo.

“Katika hospitali kadhaa nilizotembelea, nimehuzunika kuona Watoto wengi wakiteseka kutokana na utapiamlo, wengine hawatapona kama hawatapata matibabu kwa wakati” amesema Bi.Gough 
Watoto wanaoishi Haiti wapo kwenye ongezeko la hatari kubwa kutokana na mjumuisho wa mambo kadhaa ikiwemo kuzuka kwa vurugu, janga la Corona au COVID-19, ukosefu wa maji safi na salama, mazingira duni, pamoja na hali mbaya ya hewa. 

Katika kipindi cha janga la Corona, huduma za afya ziliathirika ikiwemo utoaji chanjo kwa Watoto. Kwa mujibu wa UNICEF asilimia 9.7 ya Watoto nchini Haiti hawajawahi kupata chanjo ya aina yeyote na asilimia 58 hawajapokea chanjo zote zinazotakiwa kwa Watoto. Na wale waliopokea chanjo zote, asilimia 42 wanaishi kwenye mazingira hatarishi ambako kuna uhaba wa huduma muhimu kwa Watoto na maeneo mengi yameathiriwa na vurugu. 

Mwaka 2020, UNICEF, serikali ya Haiti na washirika wake walitoa matibabu kwa Watoto 33,372. Kwa mwaka huu wa 2021, UNICEF ndani ya wiki chache kutoka sasa itaishiwa chakula chenye virutubisho kilicho tayari kinachotolewa kwa Watoto kutokana na uhaba wa fedha.

“UNICEF inahitaji kwa haraka jumla ya Dola za kimarekani Milioni 3 kwa ajili ya kununua mahitaji muhimu na dawa ili program ya kuwasaidia Watoto iweze kuendelea, iwapo fedha hizi hazitapatikana maelfu ya Watoto watakosa huduma wanazopatiwa kwa sasa za kuokoa maisha yao", amesisistiza Gough.

Kwa mwaka 2021, UNICEF inatafuta Dola za kimarekani milioni 48.9 ili kuweza kusaidia mahitaji ya kibinadamu yanayohitajika na watu milioni 1.5 nchini Haiti ambao kati yao zaidi ya 700,00 ni Watoto, hali ambayo imezidi kuwa mbaya kutoka na janga la COVID-19. Hadi sasa maombi haya ya msaada wa kibinadamu ni kama hayajasaidiwa kabisa 

 

♦ Kurambaza ukurasa mahsusi wa Siku ya Kiswahili Duniani bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Utapiamlo mkali|COVID-19|Corona

Taarifa Zihusianazo

Maafisa huko Shenzhen nchini China wakiwa katika majukumu  yao ya kawaida ya kufuatilia wagonjwa wa virusi vya Corona

WHO yaingiwa hofu na mwenendo wa maambukizi ya virusi vya Corona, COVID-19

Mtoto akiwa amekaa katika gari lililo ungua moto huko Tigray Kaskazini mwa Ethiopia

Tigray na Amhara nchini Ethiopia hali bado tete na ya wasiwasi

Mkimbizi kutoka Colombia akiwa nyumbani na mke wake kutoka Ecuador maeneo ya San Lorenzo, Ecuador.

Wakimbizi Wazee nao wanahitaji ajira ili kuweza kujikimu 

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials