Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yaimarisha msaada kwa maeneo yaliyohatarini kukumbwa na njaa 

Mtoto wa umri wa miaka mitatu akipokea mgao wa chakula kutoka WFP katika makazi ya wakimbizi wa ndani Taiz, Yemen.
© WFP/Annabel Symington
Mtoto wa umri wa miaka mitatu akipokea mgao wa chakula kutoka WFP katika makazi ya wakimbizi wa ndani Taiz, Yemen.

WFP yaimarisha msaada kwa maeneo yaliyohatarini kukumbwa na njaa 

Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP limeimarisha msaada wa chakula katika maeneo yanayokabiliwa na njaa nchini Yemen kama sehemu ya kuzuia baa la njaa lakini uwezo wa shirika hilo kuendelea na shughuli hadi mwishoni mwa mwaka ziko njia panda. 

Mkurugenzi wa WFP nchini Yemen Laurent Bukera amesema, “udhaifu wa Yemen ukijumuishwa na vichocheo vya uhakika wa chakula umeacha Yemen katika hatari ya viwango vya juu vya njaa na mazingira ya njaa. Ameongeza kwamba, ongezeko la machafuko, kudorora kwa uchumi, kupand akwa bei ya bidhaa na janga la COVID-19 vimechangia katika ongezeko la njaa kwa mwaka uliopita." 

Takriban watu 50,000 nchini Yemen wanaishi katika mazingira ya njaa na watu milioni 5 wako katika hatari. Mtu mmoja anafariki dunia katika kila dakika kumi kutokana na magonjwa yanayozulika kwa mfano kuhara, utapiamlo na mambukizi ya mfumo wa kupumua. 

WFP imerejelea kuwasilisha mahitaji ya dharura mwezi uliopita baada ya kupokea ufadhili na inafikia watu milioni sita katika majimbo tisa yaliyohatarini ikiwemo Hajjah, Al Jawf, Amran, Al Hodeidah, Raymah, Al Mahwit, Sa’ada, Dhamar na Taiz. 

Kuanzia mwezi Juni watu hawa watapokea mlo wa siku kamili kila mwezi  

Njaa imeongezeka nchini Yemen wakati mzozo ukiendelea kuongezeka, na kufurusha familia kwa mara ya tatu au nne wakati vita vikiendelea kwa mwaka was aba. 

Ongezeko la bei ya vyakula kwa asilimia hadi 200 zaidi ya viwango vya kabla ya vita na imefanya mamilioni ya watu kushindwa kununua chakula. Isitoshe awamu ya pili ya  janga la COVID-19 limepiga maeneo mengi Yemen na mfumo wa afya unashindwa kumudu. 

 Kama azimio la Baraza la Usalama la Usalama namba 2417 lililopitishwa miaka mitatu iliyopita mwezi Mei linavyosema mnyororo wa njaa na mzozo unamanisha aman ndio suluhu pekee kwa mzozo wa njaa nchini Yemen. Hadi siku hiyo, msaada wa kibinadamu ni muhimu na upungufu wa ufadhili unaweza kuwa na madhara mabaya kwa wayemeni.