Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNESCO leo imekabidhi tuzo ya Guillermo Cano kwa Maria Ressa

Picha kutoka kwenye video wakati Maria Ressa alipokuwa akishiriki mkutano wa UNESCO kuhusu uhuru wa vyombio vya habari. (Mei 4, 2020)
UNESCO
Picha kutoka kwenye video wakati Maria Ressa alipokuwa akishiriki mkutano wa UNESCO kuhusu uhuru wa vyombio vya habari. (Mei 4, 2020)

UNESCO leo imekabidhi tuzo ya Guillermo Cano kwa Maria Ressa

Utamaduni na Elimu

Mwandishi wa habari wa uchunguzi wa Ufilipino leo ametunukiwa tuzo  ya heshima kwenye hafla iliyoandaliwa iliyoandaliwa na Serikali ya Namibia na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO katika mji mkuu Windhoek, nchini Namibia ambako wataalamu wa vyombo vya habari wanataka hatua za dharura zichukuliwe dhidi ya vitisho na kudhoofishwa kwa uhuru wa habari kote ulimwenguni.

Hafla hiyo iliyofanyika leo Mei 2 na usiku wa kuamkia siku ya uhuru wa vyombo vya Habari duniani, imeandaliwa na UNESCO kwa  kushirikiana na serikali ya Namibia ili kutoa Tuzo ya Unesco ya Guillermo Cano kwa mshindi wa mwaka  2021 ambaye ni mwandishi wa habari wa Ufilipino Maria Ressa.
Tayari ameshakamatwa kwa kutumia taaluma ya mwandishi wa Habari za uchunguzi. 
Maria Ressa anaendesha wavuti wa habari, ujulikanao kama Rappler, ambao unaripoti visa vya ufisadi na makosa.
Tuzo hiyo ya UNESCO ya dola 25,000 imeanzishwa ili kumuenzi mwandishi wa Habari wa Colombia aliyeuawa