Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Mhudumu wa afya akijaza bomba na dozi ya chanjo katika kambi ya warohingya ya Cox's Bazar nchini Bangladesh.
© UNICEF Patrick Brown
Mhudumu wa afya akijaza bomba na dozi ya chanjo katika kambi ya warohingya ya Cox's Bazar nchini Bangladesh.

UNICEF kuandaa sindano na mabomba ya utoaji chanjo dhidi ya COVID-19 

UNICEF kuandaa sindano na mabomba ya utoaji chanjo dhidi ya COVID-19 

Mhudumu wa afya akijaza bomba na dozi ya chanjo katika kambi ya warohingya ya Cox's Bazar nchini Bangladesh.
© UNICEF Patrick Brown
Mhudumu wa afya akijaza bomba na dozi ya chanjo katika kambi ya warohingya ya Cox's Bazar nchini Bangladesh.
19 Oktoba 2020
Afya

Wakati duniani inasubiri kwa hamu chanjo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICF, nalo limeanza maandalizi ya kuhakikisha chanjo hiyo inatolewa na kusambazwa mapema na kwa usalama kwa kununua na kuhifadhi mabomba ya sindano na vifaa vingine vya kufanikisha zoezi hilo.

Taarifa ya UNICEF iliyotolewa leo jijini New York, Marekani imesema kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa kuwa punde tu baada ya chanjo hiyo kukamilika majaribio yake na kuthibitika iko salama kwa matumizi, dunia itahitaji mabomba mengi ya sindano sambamba  na dozi zenyewe. 

Katika kuanza maandalizi hayo, UNICEF itahifadhi kwenye bohari zake mabomba milioni 520 ya sindano ili kuhakikisha ifikapo mwishoni mwa mwaka 2021 ina mabomba bilioni 1 kwa lengo ya kwamba mabomba yanayotakiwa yanafikia nchi zinazoyahitaji kabla ya chanjo kufika. 

UNICEF inasema kuwa katika kipindi cha mwaka 2021, kwa kutarajia kuwa kuna chanjo za kutosha za COVID-19, shirika hilo linatarejia kusambaza zaidi ya mabomba bilioni 1 ya sindano kwa ajili ya utoaji wa chanjo ya COVID-19, ikiwa ni kando ya mabomba milioni 620 ambayo UNICEF itakuwa imenunua kwa ajili ya chanjo zingine kama vile surua na homa ya matumbo. 

Akizungumzia mpango huo wa UNICEF, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo Henrietta Fore amesema, “kupatia chanjo wakazi wa dunia dhidi ya COVID-19, itakuwa ni kazi kubwa katika historia ya binadamu, na tutahitaji kufanya kazi kwa haraka kadri chanjo hiyo inavyotengenezwa. Ili kwenda haraka, tunalazimika kuanza kazi hiyo kwa haraka sasa. Mwishoni mwa mwaka huu, tutakuwa tayari kuna mabomba nusu milioni ya kutolea chanjo yakiwa tayari yamehifadhiwa ambako yatasambazwa haraka na kwa gharama nafuu. Kiwango hicho kinatosha kwa kukidhi dunia mara moja na nusu.” 

  Kando mwa mabomba ya sindano, UNICEF pia inanunua makasha milioni 5 salama yatakayotumika kutupia mabomba na sindano zilizotumika kwenye vituo vya afya, lengo likiwa ni kuepusha majeraha yanayoweza kutokana na kuchomwa na sindano na pia kusambaza magonjwa kwa njia ya damu. 

Kila kasha moja linachukua mabomba na sindano 100 na kwamba makasha hayo yanaweza kuhifadhiwa kabla ya matumizi kwa miaka 5. 

Shirika hilo limesema kwa upande wa chanjo ili kuhakikisha inasafirishwa salama na katika kiwango cha joto kinachotakiwa, tayari kwa kushirikiana na shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, wanapanga mpango wa kupata mifumo ya usafirishaji na uhifadhi wa bidhaa kwa ubaridi kwa ubia na sekta ya umma na binafsi. 

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
COVID-19|chanjo|Coronavirus

SIKILIZA RADIO YA UMOJA WA MATAIFA

    Taarifa Zihusianazo

    Muuguzi akiandaa chanjo ya kuchanja mtoto katika kliniki Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

    COVID-19  yakosesha watoto huduma muhimu ya chanjo

    UNICEF ikifikisha shehena ya chanjo dhidi ya COVID-19 nchini Msumbiji

    Mwaka mmoja wa janga la COVID-19 kuna nuru gizani:Guterres

    Mtu akipatiwa chanjo (Maktaba)

    Tumeanza rasmi chanjo ya majaribio ya dhidi ya COVID-19: WHO

    Maktaba

    • Taarifa kwa watangazaji
    • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
    • Angalizo
    • UN Journal
    • Taarifa za Habari
    • Mikutano
    • Maktaba ya Picha na Video
    • Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu

    • Taarifa zote
    • Safari za kiofisi
    • Kona ya wanahabari
    • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

    Msemaji wa UN

    • Nyaraka zote
    • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
    • Maandishi ya mkutano na wanahabari
    • Taarifa kwa wanahabari

    Tupate

    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • RSS
    • Mawasiliano
    • Rambaza
    • Washirika wetu kwa sasa
    Umoja wa Mataifa
    Changia
    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • Soundcloud
    • Podcast
    • UN Social Media
    • A-Z Site Index
    • Hakimiliki
    • Maswali ya mara kwa Mara
    • Fraud Alert
    • Privacy Notice
    • Kanuni za matumizi
    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • SoundCloud
    • Podcast
    • More Socials