Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Wanawake waliofurushwa makwao wakiwa katika kambi ya Awaradi nchini Niger.
© UNOCHA/Eve Sabbagh
Wanawake waliofurushwa makwao wakiwa katika kambi ya Awaradi nchini Niger.

Vita na janga la COVID-19 vyawaweka watoto katika hali mbaya Sahel:UNICEF

Vita na janga la COVID-19 vyawaweka watoto katika hali mbaya Sahel:UNICEF

Wanawake waliofurushwa makwao wakiwa katika kambi ya Awaradi nchini Niger.
© UNOCHA/Eve Sabbagh
Wanawake waliofurushwa makwao wakiwa katika kambi ya Awaradi nchini Niger.
16 Oktoba 2020
Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limesema vita vya silaha na athari za kiuchumi na kijamii zilizosababishwa na janga la corona au COVID-19 vimefanya hali ya Watoto kuwa mbaya zaidi katika ukanda wa Sahel.

Kwa mujibi wa taarifa ya shirika hilo iliyotolewa leo mjini Geneva Uswis, “Watoto milioni 7.2 nchini Burkina Faso, Mali na Niger sasa wanahitaji msaada wa kibinadamu ikiwa ni ongezeko la theluthi mbili ndani ya mwaka mmoja. 

Zaidi ya Watoto milioni moja kati ya hao wamelazimika kukimbia makwao na kutawanywa, huku huduma muhimu kama maji salama kwa ajili ya kuwawezesha Watoto hao kuishi  na kuzuia kusambaa kwa gonjwa la COVID-19  sasa ni adimu hususani miongoni mwa watu waliotawanywa.” 

Taarifa hiyo imesema makadirio ya idadi ya Watoto wataugua utapiamlo mwaka huu yameongezeka kwa asilimia 5. Hali imeelezwa kuwa mbaya zaidi hasa katika baadhi ya majimbo ya Burkina Faso ambayo yanahifadhi wakimbizi na wakimbizi wa ndani .  

Na katika jamii za Djibo, Gorgadji na Barsalogho idadi ya vifo miongoni mwa Watoto tayari imeshapita kiwango cha hatari. UNICEF inasema “katika nchi hizo tatu mashambulizi ya kulenga yamesababishwa kufungwa kwa shule zaidi ya 4000 kabla ya janga la COVID-19 kufunga zilizosalia. Pia kumekuwa na uthibitisho wa ukiukwaji mkubwa wa haki za Watoto ikiwemo kuwaingiza vitani kwenye mapigano, ubakaji na ukatili wa kingono pia umeongezeka kwa akiasi kikubwa hususan Mali.” 

UNICEF imesisitiza kuwa ili Sahel ya Kati iweze kujikwamua kutokana na migogo hii basi lazima nchi hizo zihakikishe kwamba Watoto wa kizazi hili wanaweza kupindua ukurasa wa machafuko na umasikini uliokithiri, lakioni kwa sasa ukanda huo unahitaji msaada ili kuhakikisha vifo zaidi haviendelei na hali haigeuki kuwa janga kubwa la kibinadamu. 

UNICEF ikishirikiana na wadau wanajitahidi kuwamikia mamilioni ya Watoto kwa misaada ya kuokoa maisha, chakula, chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali na fursa za kupata maji safi na usafi. 

Hata hivyo shirika hilo linasema changamoto kubwa ni fedha kwani hadi sasa limepokea asilimia 31 tu yad ola milioni 210 inazohitaji kwa ajili ya kutoa msaada wa kibinadamu kwa mwaka huu kwenye ukanda wa Sahel. 

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Sahel|vita|COVID-19|msaada wa kibinadamu

Taarifa Zihusianazo

Mvulana mchanga ambaye alilazimika kukimbia nyumbani kwao kutokana na vurugu huko Kaya, Burkina Faso.

Muda unawatupa mkono watu wa Sahel wakati mashambulizi yakishika kasi:UNHCR

Familia eneo   la Kaya jimbo la Sanmatenge nchini Burkina Faso ikipata mlo baada ya kupokea mgao kutoka WFP.

Watu milioni 24 wanahitaji msaada wa kuokoa maisha Sahel:OCHA

Familia ikipokea msaada wa chaakula katika kituo cha kusambaza chakula huko Ras al'Arah huko Lahj Governorate nchini Yamen

Wahisani wa kimataifa wakutana kuchangisha fedha kuinusuru Yemen:UN

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials