Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Mtoto wa miaka mitano akiwa amelala sakafuni kwenye jengo la enzi za kikoloni linalowahifashi wakimbizi kambi ya Izinga Boga, DRC
© UNICEF/Roger LeMoyne
Mtoto wa miaka mitano akiwa amelala sakafuni kwenye jengo la enzi za kikoloni linalowahifashi wakimbizi kambi ya Izinga Boga, DRC

Maelfu ya watoto waendelea kuwa hatarini Ituri DRC:UNICEF 

Maelfu ya watoto waendelea kuwa hatarini Ituri DRC:UNICEF 

Mtoto wa miaka mitano akiwa amelala sakafuni kwenye jengo la enzi za kikoloni linalowahifashi wakimbizi kambi ya Izinga Boga, DRC
© UNICEF/Roger LeMoyne
Mtoto wa miaka mitano akiwa amelala sakafuni kwenye jengo la enzi za kikoloni linalowahifashi wakimbizi kambi ya Izinga Boga, DRC
6 Oktoba 2020
Amani na Usalama

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limesema linaendelea kutiwa hofu kubwa kuhusu maelfu ya watoto walio hatarini wakati huu machafuko yakiendelea kwenye jimbo la Ituri Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC. 

Kwa mujibu wa taarifa ya shirika hilo iliyotolewa leo watoto wanaendelea kuteseka kwa sababu ya machafuko na vurugu zilizosababishwa na vita vya muda mrefu katika jimbo hilo.

UNICEF inasema machafuko yalishika kasi mwanzoni mwa mwaka huu wa 2020 na tangu hapo hali kwa maelfu ya Watoto jimboni Ituri imezidi kuzorota. 

“Mashambulizi ya wanamgambo katika maeneo ya raia yamesababisha mamia ya vifo na UNICEF imepokea taarifa za watoto kujeruhiwa, kuawa au kuingizwa kwenye mapigano na makundi yenye silaha.Wakati huohuo zaidi ya watu milioni 1.6 wengi wao wakiwa ni wanawake na Watoto wanakadiriwa kuwa wakimbizi wa ndani kutokana na mchafuko hayo.” 

 

Athari za machafuko hayo 

 

Kwa mujibu wa UNICEF kati ya Januari na Juni 2020, watoto 91 wameuawa, 27 kujeruhiwa na 13 ni waathirika wa ukatili wa kingono. 

Pia karibu vituo 18 vya afya vimeporwa au kuharibiwa wakati mashambulizi dhidi ya shule 60 yamewaacha Watoto takriban 45,000 bila madarasa. 

Haya ni matukio yaliyothibitishwa lakini idfadi kamili huenda ikawa kubwa zaidi. Limesema shirika la UNICEF. 

Jimboni Ituri shirika hilo linasema hivi sasa kuna watu milioni 2.4 wanaohitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.  

Watu 150,000 wakiwemo Watoto 87,000 wamepatiwa msaada na UNICED na washirika wake hasa katika masuala ya huduma za afya na lishe, ulinzi, elimu, maji na usafi kati ya Januari na Agosti mwaka huu. 

 

Msaada mwingine uliotolewa  

 

Zaidi yah apo UNICEF na washirika wake pia wamewasaidia Watoto 365 ambao awali walikuwa wakihushwa na makundi ya wanagambo na yenye silaha kuweza kurejea na kujumuishwa katika jamii, kuwasafa ndugu wa familia zao na kuwapa msaada wa kisaikolojia. 

Watoto wengine 87,000 walio hatarini wamepewa fursa ya maeneo ya jamii ambako wanaweza kucheza na kujifunza. 

Kwa Watoto 68 waathirika wa ukatili wa kingono UNICEF imehakikisha wamepatiwa huduma za afya na msaada wa kisaikolojia na kisheria. 

Na kwa waathirika wengine 140,000 wa machafuko yanayoendelea wakiwemo Watoto 85,000 wanaendelea kupokea msaada wa vifaa ambavyo si chakula, malazi na vifaa vya usafi na kujisafi. 

Hata hivyo UNICEF imesema usalama mdogo kwenye jimbo la Ituri na ukata wa fedha vimeendelea kuathiri shughuli za misaada , huku ombi la UNICEF la dola milioni 318 lina pengo la asilimia 74 ambayo ni saw ana dola milioni 235. 

 

 

♦ Kurambaza ukurasa mahsusi wa Siku ya Kiswahili Duniani bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
watoto|DRC|Ituri|machafuko

Taarifa Zihusianazo

Machafuko katika jimbo la Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC yansababisha watu kukimbilia nchi jirani.

Miezi miwili baada ya machafuko, hofu yaendelea kutawala Ituri DRC

Wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakivuka ziwa Albert kuelekea Uganda.

Zaidi ya raia 5,000 wakimbia DRC wakati wa msimu wa Krismasi

Anwarita akiwa nyumbani kwa wazazi wake walezi huko Bona, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

"Nilisikia sauti usiniache! ndipo nikakuta mtoto Anuarita"- Asema baba aliyenusuru mtoto msituni huko DRC

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials