Wauguzi na wakunga huduma ya usafi iko mikononi mwenu:WHO
Wauguzi na wakunga huduma ya usafi iko mikononi mwenu:WHO
Katika kuadhimisha siku ya usafi wa mikono hii leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linawachagiza watu kote duniani kuongeza juhudi za kuhakikisha usafi wa mikono katika vituo vya afya ili kuwalinda wahudumu wa afya na wagonjwa dhidi ya maambukizi.
Shirika la WHO linasema maadhimisho ya mwaka huu yanajikita na kaulimbiu “Okoa maisha:wauguzi na wakunga huduma ya usafi iko mikononi mwenu” ikienda sanjari na mwaka wa wauguzi na wakunga na lengo kuu ni kutambua mchango wa wahudumu hao wa afya kama mashujaa walio msitari wa mbele, kuwashukuru na kutanabaisha jukumu kubwa walilonalo katika kuzuia maambukizi .
Elizabeth Iro ni mkuu wa wauguzi katika shirika la WHO anaeleza sababu ya kuihusisha siku ya mwaka huu na wauguzi na wakunga.
“Sio tu kwamba tunataka kuchagiza usafi wa mikono , kuzuia maambukizi na hulka ya kuyadhibiti lakini pia tunataka kutambua jukumu muhimu walilonalo wauguzi na wakunga katika kuzuia maambukizi yanayoweza kuepukika”
Ameongeza kuwa wauguzi na wakunga ni muhimu sana kwani
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.“Kama kundi kubwa kabisa la wahudumu wa afya wanaotoa huduma kwa wagonjwa, wauguzi na wakunga ni muhimu katika kutoa huduma ya usafi. Katika nchi nyingi wanaoongoza katika kudhibiti maambukizi ni wauguzi hivyo wana nafasi kubwa katika kuzuia maambukizi hayo”
Na kuhusu kuzingatia usafi wa mikono Elizabeth anasema
“Usafi wa mikono ni hatua moja muhimu na inayofanyakazi unayoweza kuichukua kupunguza kusambaa kwa vijidudu na kuzuia maambukizi, ikiwemo virusi vya COVID-19”
Siku ya usafi wa mikono ilianza kuadhimishwa rasmi mwaka 2009 na tangu hapo hufanyika kila mwaka tarehe 5 Mei.