Kenya yaendelea kuchukua hatua huku idadi ya wagonjwa wa Corona ikifikia 281
Huku vita dhidi ya viuusi vya corona vikipamba moto kote duniani, huko Kenya sasa idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo imefika watu 281. Hii ni baada ya wagonjwa wengine 11 kuthibitishwa hii leo. Hata hivyo wizara ya afya nchini humo imetangaza kuwa itawafanyia watu zaidi uchunguzi kila siku kubaini ni maeneo yapi yaliyoathirika kwa kiwango kikubwa. Jason Nyakundi anayo taarifa zaidi
Wizara ya afya nchini Kenya imetangaza kuwa vituo vya kuwafanyia watu uchuguzi dhidi ya virus vya korona vitaongezwa ambapo kila kaunti itakuwa na takriban mahabara moja.
Akiongea na waandishi wa habari waziri wa afya mutahi kagwe alisema vituo 33 vya karantini kote nchini Kenya kwa sasa vinawazuia jumla ya watu 483.
Bw Kagwe amesema watu wengine 455 wamewekwa katika karantini ya lazima baada ya kukiuka amri ya serikali ya kuwataka kubaki manyumbani mwao hasa usiku.
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.Waziri amewaonya wale wanaokiuka amri za serikali wakati zinapoendelea jitihada za kupambana na virusi hatari vya corona.
Wakati huo huo idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya corona hadi sasa imeongezkea hadi watu 281 kufuatia kuthibitishwa wagonjwa 11 zaidi.
Kati ya hao 11, 5 ni wanawke na 6 wanaume wote walio kati ya umri wa miaka 11 na 80.
Waziri Kagwe amesema saba kati ya wagonjwa wako Mombasa huku wanne wakiwa Nairobi.
Kagwe pia ametangaza kuwa wagonjwa 2 zaidi, kati yao akiwa ni daktari wamepona na kufikisha idadi ya wagonjwa waliopona virusi vya korona nchini Kenya kuwa watu 69
Hadi sasa jumla ya watu 14 wamefaraki kutokana na virusi vya Corona nchini Kenya.