Chuki na unyanyapaa vimeongezeka wakati huu wa COVID-19:Achiume
Chuki na unyanyapaa vimeongezeka wakati huu wa COVID-19:Achiume
Mtaalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa dhidi ya masuala ya ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni , ubaguzi na hali zingine za kutovumiliana profesa Tendayi Achiume amesema wakati huu wa janga la virusi vya Corona au COVID-19 hali hizi zimedhihirika kuongezeka.
Akizungumza na UN News Bi.Achiume amesema makundi yanayolengwa na ubaguzi na chuki hizo ni yale ambayo kwa muda mrefu yamekuwa waathirika wa vitendo hivyo vya kibaguzi,“Katika hali ya dharura kama hii mara nyingi matatizo ambayo yalikuwepo yanaongezeka , makundi memgi ni yale ambayo tayati yalikuwa yanakabiliwa na ubaguzi, chuki na hali ya kutovumiliana chukulia mfano Waasia wenye asili Marekani hivi sasa , Waafrika ambao wanakabiliwa na hatua mbalimbali China hivi sasa kwa ajili ya kukabiliana na COVID-19, wafikirie Waroma ambao wanalengwa katika nchi mbalimbali za Ulaya wakishutumiwa kusambaza virusi na kukabiliwa na hatua kali.”
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.Amesema hata katika masuala muhimu kama upimaji kwa mfano kuchagua nani apimwe badala ya kuzingatia sayansi na hali halisi inaruhusuubagui huo kupanua wigo n ahata kuingia kwenye sera haki ambayo inaiweka jamii nzima kwenye changamoto na hilo ni tatizo kubwa. Na je changamoto ni ipi katika kukabiliana na ubaguazi na unyanyapaa huu hasa wakati huu wa COVID-19 Bi. Achiume anasem, “Sehemu ya changamoto ni kuwafanya watu kuwaona watu wengine kama binadamu na pia kuoanisha jinsi wewe unavyokabiliwa na ubaguzi na wengine wanavyokabiliwa na ubaguzi”
Ameongeza kuwa Pamoja na serikali, viongozi wa kijamii na sekta mbalimbali vyombo vya Habari pia vina wajibu mkubwa katika kupambana na ubaguzi na chuki kuanzia kwenye vyombo vya Habari vya kawaida hadi kwenye mitandao ya kijamii. Nini kifanyike sasa kuhakikisha jamii nayo inatambua na kuachana na ubaguzi?“Nadhani elimu ndio suluhu hapa , kuwaona watu wengine kama watu , makundi mengine kama binadamu , ndio itakuwa vigumu kujihusisha na vitendo hata vidogo vya ubaguzi. Napenda kuamini hivyo na kama sivyo basi tuko kwenye tatizo kubwa.”