Kwenye vita watu milioni 100 wako hatarini kwa COVID-19:OCHA
Kwenye vita watu milioni 100 wako hatarini kwa COVID-19:OCHA
Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masula ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA “Dunia ni lazima iendelee kuwasaidia wasiojiweza ikiwemo kupitia msaada wa kibinadamu unaoratibiwa na Umoja wa Mataifa na mpango wa msaada kwa wakimbizi.”
Jens Laerke ambaye ni msemaji wa OCHA ameongeza kuwa kwa ujumla mashirika ya misaada yanahofia kuhusu upungufu wa mifumo ya ufuatiliaji katika baadhi ya nchi ambako maelfu ya watu wasiojiweza wanaishi. “Nchi hizi huenda hazina miundombinu ya kukabiliana na athari kubwa za mlipuko huo wa COVID-19.”
Suala linguine amesema ni mrundikano wa makambi ya wakimbizi wa ndani katika sehemu zenye majanga ya kibinadamu hali ambayo inaleta hatari kubwa ya COVID-19. OCHA inasema watu wengi wanaishi katika mazingira magumu na hawana kabisa au wanazo kidogo sana huduma za msingi za usafi na afya.
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.“Wakati virusi vinafika katika sehemu hizi athari zake zinaweza kuwa mbaya sana. Na mlipuko mpya wa COVID-19 utaongeza gharama kubwa kwa maisha ya wat una jamii hasa ambazo kwa sasa zinakabiliwa na matatizo mengine ya kiafaya kama surau na homa ya manjano ambayo hayapatiwi uzito mkubwa.”
UN yaomba ufadhili wa fedha wiki ijayo
Zaidi ya changamoto zote hizo athari katika mnyororo wa usambazaji inamaanisha kwamba lishe ya kukabiliana na utapiamlo inayozalishwa katika nchi moja inaweza isifike katika nchi nyingine ambako inahitajika.
Kwa sasa mashirika ya misaada ya kibinadamu yanajiandaa kusitisha program za mlo mashuleni. OCHA inasema pia maji na usafi vinaweza visitosheleze au kutopatikana kabisa. “Vituo vya usambazaji wa misaada ambako watu wengi hukusanyika kwa ajili ya chakula au misaada mingine huenda ikakatazwa na suluhu mbadala zitahitajika.”
Bwana Laerke amesema katika hali hii lengo la jumuiya ya misaada ni kuendelea kutoa msaada muhimu wa kuokoa maisha huku ikichukua hatua Madhubuti kuepuka zjanga kubwa linaloweza kusababishwa na COVID-19 kwa watu hawa wenye uhitaji mkubwa.
Kwa sasa mashirika ya Umoja wa Mataifa yanatathimini wapi operesheni za kibinadamu zinapatwa na dosari na kuweza kusaka suluhu.
Pia Umoja wa Mataifa unalifanyia kazi suala la mpango thabiti wa masuala ya kibinadamu ambao unatarajiwa kuzinduliwa wiki ijayo.
“Ili kuikomesha COVID-19, inabidi kuikomesha kila mahali.Endapo hatutokomesha maambukizi duniani kote , virusi vinaweza kurejea kwenye nchi ambazo zilidhani ziko salama” limesisitiza shirika la OCHA na kuongeza kwamba kuendelea na hatua za kibinadamu kukabiliana na janga hili ni kitendo cha mshikamano wa kimataifa na pia ni ishara ya ubinadamu.