Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwaka 2017-2019

Kutoka kushoto: Watu wavuka Myanmar kuenda Cox's Bazar, kusini mashariki mwa Bangladesh; Walinda amani wanaoshirikiana na Misheni ya UN nchini Liberia watimisha azma yao; Mwanaharakati wa miaka 8 wa India Licypriya Kangujam akiwa COP25.
UN Photo.
Kutoka kushoto: Watu wavuka Myanmar kuenda Cox's Bazar, kusini mashariki mwa Bangladesh; Walinda amani wanaoshirikiana na Misheni ya UN nchini Liberia watimisha azma yao; Mwanaharakati wa miaka 8 wa India Licypriya Kangujam akiwa COP25.

Mwaka 2017-2019

Amani na Usalama

Mwaka 2017 ulianza kwa Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuanza rasmi hatamu yake ya uongozi na kuahidi kuleta mabadiliko katika usawa wa kijinsia na kuzuia mizozo katika dunia yenye migawanyiko.

“Tuko duniani iliyogawanyika, tunahitaji kuwa dunia iliyoungana.”

Janga kubwa lilishuhudiwa nchini Myanmar ambapo jamii ya warohingya laki sita walilazimika kukimbia makwao kuelekea Bangladesh ambako miundombinu imezidiwa uwezo.

Wakimbizi wa Rohingya kutoka Mynamar ambao sasa wanaishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Cox's Bazar nchini Bangladesh wakiwa wanajindaa kukabili msimu wa mvua kwa kujenga kutumia mianzi.
© UNHCR/Caroline Gluck
Wakimbizi wa Rohingya kutoka Mynamar ambao sasa wanaishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Cox's Bazar nchini Bangladesh wakiwa wanajindaa kukabili msimu wa mvua kwa kujenga kutumia mianzi.

 

Nchini Yemen watu milioni 8.5 wako katika hatari ya ukame mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa.

Mwaka huu pia kulikuwa na shambulio baya dhidi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa kushuhudiwa kwa miongo kadhaa lililosababisha watu wengi zaidi kupoteza maisha ambapo walinda amani 14 kutoka Tanzania waliuwawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC. Balozi Modest Mero ni mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa wakati huo alisema

"Sisi kama watanzania  tutaendelea kuendeleza amani kwa sababu uwezo tunao na nia tunayo , na pia na sehgemu ambayo sisi tumejitoa kimataifa kwamba tutalinda amani dunianani na hatuwezi kuwacha."

Takriban wahamiaji laki moja walivuka baharí ya Mediterranea kueleka Ulaya huku wahamiaji takriban 3,000 wakizama na kupoteza maisha wengi wakikimbia machafuko na hali mbaya ya kiuchumi kusini mwa jangwa la Sahara.

Mwaka 2018

Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Liberia UNMIL Machi 30  ulifunga rasmi milango baada ya kuhudumu kwa miaka 15

Kamanda wa kwanza mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Liberia UNMIL Luteni Jenerali mstaafu Daniel  Ishmael Opande akiwa katika moja ya operesheni za Umoja wa Mataifa mjini Monrovia.
Picha na UN
Kamanda wa kwanza mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Liberia UNMIL Luteni Jenerali mstaafu Daniel Ishmael Opande akiwa katika moja ya operesheni za Umoja wa Mataifa mjini Monrovia.

 

UNMIL uliweka mazingira mazuri kiusalama yaliyowawezesha zaidi ya wakimbizi milioni moja na watu waliofurushwa kurejea nyumbani, uliunga mkono chaguzi tatu za rais na kusaidia serikali kuunda mamlaka kote nchini kufuatia miaka ya mapigano na ukosefu wa usalama.

Mwaka 2018 Umoja wa Mataifa na kwingineko watu walikusanyika kumuaga aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan kufuatia kifo chake Agosti 18.

 

Picha ya Kofi Annan alipoteuliwa kwa muhula wa pili kama Katibu Mkuu wa UN 1 Januari 2002 na kumaliza  31 Disemba 2006.
UN Photo.
Picha ya Kofi Annan alipoteuliwa kwa muhula wa pili kama Katibu Mkuu wa UN 1 Januari 2002 na kumaliza 31 Disemba 2006.

Mwaka 2019 Katibu Mkuu aliongoza mkutano wa ngazi ya juu wa viongozi wa Umoja wa Mataifa kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi ambapo katika kikao hicho mwanaharakati kijana wa mazingira kutoka Sweden Greta Thunberg hakuficha hasira zake kutokana na hali ya sasa,

Anasema, “mmeiba ndoto zangu na utoto wangu kwa maneno matupu na mimi ni miongoni mwa walio na bahati, watu wanakabiliwa na madhila. Watu wanakufa. Mfumo wa ikolojia unakufa. Tuko katika mwanzo wa kutokomea, na kile ambacho mnaweza kuzungumzia ni maswala ya fedha na hadithi kuhusu ukuaji wa milele wa uchumi. Mnathubutu vipi?”

Mwanaharakati wa mazingira kutoka Sweden, Greta Thunberg akizungumza wakati wa kongamano la hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi mwaka 2019.
UN Photo/Cia Pak
Mwanaharakati wa mazingira kutoka Sweden, Greta Thunberg akizungumza wakati wa kongamano la hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi mwaka 2019.

 

Kuelekea mwaka ujao Umoja wa Mataifa unatimiza miaka 75 tangu kuasisiwa na ili kuadhimisha siku hiyo kutazinduliwa majadiliano ya 75 ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya sayari dunia tunayoitaka