Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Dola 5000 zamsubiri mshindi wa uhifadhi wa mazingira Tanzania

Maonesho na ubunifu wa mavazi ni moja ya vyanzo vya mapato kwa wajasiriamali.
UN Photo/Manuel Elías
Maonesho na ubunifu wa mavazi ni moja ya vyanzo vya mapato kwa wajasiriamali.

Dola 5000 zamsubiri mshindi wa uhifadhi wa mazingira Tanzania

Tabianchi na mazingira

Wakati nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP25 wakikutana huko Madrid, Hispania, nchini Tanzania mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na wadau wameaandaa maonyesho ya siku mbili yatakayoleta pamoja wajasiriamali wanaotekeleza miradi mbalimbali ya kukabiliana au kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza na waandishi wa  habari hii leo mjini Dar es salam, Tanzania, mwakilishi wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP nchini humo Clara Makenya amefafanua kwa kina..

(Sauti ya Clara Makenya)

Bi. Makenya ameenda mbali zaidi kufafanua zawadi kwa mshindi..

(Sauti ya Clare Makenya)

Maonyesho hayo yameandaliwa na shirika la kazi duniani, ILO, UN Global Compact, UNEP na chama cha warejelezaji Tanzania, TaRA.