Masharti ya taasisi za kifedha yana mchango katika kukandamiza haki za binadamu-Mtaalamu wa UN
Masharti ya maadili yanayowekwa na taasisi za kimataifa za kifedha kama vile shirika la fedha duniani IMF, mara kwa mara yanasababisha ukikukwaji wa haki za binadamu, amesema mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu madeni ya nje na haki haki za binadamu Bwana Juan Pablo Bohoslavsky katika ripoti yake itakayowasilishwa kwa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa mwezi Oktoba.
Akiongea hii leo mjini Geneva Uswisi, Bwana Bohoslavsky amesema,“Ingawa masharti yanaweza kuwa njia ya udhibiti dhidi ya matumizi mabaya ya rasilimali, ni muhimu kukumbuka kuwa masharti ya uadilifu yanathiri makundi tofauti katika jamiii na kwa namna tofauti hususani wale walioko hatarini na pia waliotengwa.”
Pia ameongeza kuwa, “ingawa mataifa ndio dhamana kuu ya haki za binadamu, taasisi za kifedha za kimataifa zinaweza kuwajibika ikiwa wataweka sera ambazo zina matokeo mabaya kwa haki za binadamu.”
Bwana Bohoslavsky anahoji, “kama taasisi za kimataifa za fedha zinaweza kuwajibishwa kwa madhara yanayozuilika yaliyosababishwa na bwawa lilijengwa kwa ufadhili wao, kwa nini wasiwajibike kwa madhara yanayozuilika dhidi ya haki za binadamu yaliyotokana na sera mbaya za kiuchumi?.”
Sheria ya kimataifa ya haki za binadamu inazuia nchi kulazimishwa kulipa madeni yake yote kwa ukamilifu kwa gharama ya kuongezeka kwa vifo vya wa watoto, ukosefu wa ajira na utapiamlo.