Michezo haichagui wala kubagua mkimbizi:Nshimirimana mkimbizi wa Burundi
Michezo haichagui wala kubagua mkimbizi:Nshimirimana mkimbizi wa Burundi
Michezo ni jukwaa ambalo hukutanisha, huunganisha na kuwaleta pamoja watu licha rangi, jinsia au hata watokako na hali zao za maisha. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa michezo ni daraja la amani na wanaichagiza katika maeneo yenye mizozo kwa ajili ya nguvu yale. Na leo inatupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, kukutana na timu ya wasichana watupu wakimbizi toka Burundi wanaosakata kabumbu.
Kutana na timu ya Morning star au nyoota ya asubuhi , walikimbia machafuko Burundi mwaka 2015 na kuhamia katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , wakiwa ukimbizini walibaini mapenzi yao ya kusakata kambumbu, wote wakiishi katika kambi ya wakimbizi ya Lusenda. Kapteni wa timu hiyo ni Emarance Nshimirimana na mchezaji mwenzie ni Speciose Nibigira
SAUTI YA NSHIMIRIMANA NA NIBIGIRA
Licha ya kutokuwa na uwanja maalum wa mpira wa miguu, viatu au njumu za kucheza mpira au hata mpira wao wenyewe hawaruhusu chochote kuingilia kati ndoto zao za kuwa wachezaji nyota siku moja
SAUTI MCHEZAJI 1
Nshimirimana anaongeza
SAUTI NSHIMIRIMANA
Nami nawatakia kila la heri