Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mustakabali wa hali ya kazi uko katika maamuzi yetu ya sasa- Guy Ryder

Rais Sergio Mattarela wa Italia akihudumia mkutano wa 108 wa Baraza la shirika la kazi duniani, ILO hii leo Juni 10, 2019 mjini Geneva, Uswisi.
ILO/Marcel Crozet
Rais Sergio Mattarela wa Italia akihudumia mkutano wa 108 wa Baraza la shirika la kazi duniani, ILO hii leo Juni 10, 2019 mjini Geneva, Uswisi.

Mustakabali wa hali ya kazi uko katika maamuzi yetu ya sasa- Guy Ryder

Masuala ya UM

Mkutano mkuu wa mwaka wa shirika la kazi duniani ILO umeanza hii leo mjini Geneva Uswisi ukiwakutanisha wawakilishi wa serikali mbalimbali duniani, wafanyakazi na waajiri kutoka katika nchi 187 wanachama wa ILO.

Akihutubia katika ufunguzi wa mkutano huo wa 108 unaofanyika shirika hilo la kazi likiwa katika mwaka wa 100 tangu kuanzishwa, Mkurugenzi Mkuu wa ILO Guy Ryder amesema, “mstakabli wa kazi utakuwa matokeo ya maamuzi yetu, machaguo yetu, uwezo wetu wa kuyafuatilia, utashi wetu kushirikiana pamoja kufanya mstakabali wa kazi ambao tunautaka.”

Aidha bwana Ryder amewaeleza wajumbe wa mkutano kuwa wako hapo kwa sababu wana maono na ujasiri sawa na Albert Thomas ambaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa kwanza wa ILO na kwamba, “ni katika uwezo wetu kutengeneza masharti ya kazi bora kwa ajili ya wote, ambamo makampuni yatastawi, watu watafanikiwa na jamii zitaendelea. Hali ambayo inahakikishia kuendelea kwa maono ya miaka 100 ya waanzilishi wa ILO.”

“Mstakabali wa kazi, hautaamliwa kwa ajili yetu, siyo na roboti na siyo na akili bandia. Ukweli ni kuwa mstakabali wa kazi utakuwa matokeo ya maamuzi yetu.” Amesisitiza bwana Ryder.

Katika siku zinazofuata za mkutano huu, zaidi ya wakuu 40 wa serikali kutoka kote duniani watahutubia mkutano huo wa kimataifa wa 108 kuhusu kazi, ambao pia unafahamika pia kama bunge la la kazi la dunia.