Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN yaunga mkono Mkataba wa Hodeida (UNMHA)

Bandari ya Hudeidah katika Yemen ni moja wa bandari inayosadia watu wa huko kwa kushughulikia misaada ya kibinadamu pamoja na mafuta.
UNICEF/Abdulhaleem
Bandari ya Hudeidah katika Yemen ni moja wa bandari inayosadia watu wa huko kwa kushughulikia misaada ya kibinadamu pamoja na mafuta.

UN yaunga mkono Mkataba wa Hodeida (UNMHA)

Amani na Usalama

Vikosi vya Umoja wa Mataifa pamoja na vikosi vya ulinzi wa pwani nchini Yemeni  vimeanza doria rasmi ya maeneo ya bandari katika mji wa Hudayidah nchini Yemeni kufuatilia makubaliano kati ya majeshi ya Houthi yaliyo chini ya uongozi Ansar Allahna  na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kuhusu mkataba wa Hodeida (UNMHA).

Hakikisho rasmi llimetolewa naUmoja wa Mataifa kuhusu  makubaliano hayo yatakayoanza  tarehe 14 mwezi mei na mkataba huo utajikita na uondoaji wa vikosi vya kijeshi na uteguzi wa mambomu ya ardhini katika bandari tatu na  katika mji wa Hodeida

Luteni Mkuu Michael Lollesgaard  amabye ni mwenyekiti wa Kamati ya ushauri wa zoezi la uondoaji wa majesji ya Houthi anasisitiza kuwa hatua hii ni sehemu ya kwanza ya makubaliano ya awali ya  uondoaji bikosi kaika mji Hodeida, kwa mujibu wa Mkataba wa Stockholm.

Serikali ya Yemeni imeihakikisha Umoja wa Mataifa  kwamba ipo tayari kuwajibika kwa sehemu yake katika awamu ya kwanza pindi itakapoombwa kufanya hivyo. Majadiliano  kati ya pande zote katika mgogoro huo nchini Yemeni yanaendelea.