Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msaada wa haraka wahitajika kwa wakimbizi nchini Sri Lanka baada ya mashambilizi -UNHCR

Bendera ya Sri Lanka (katikati) ikipepea katika viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Loey Felipe
Bendera ya Sri Lanka (katikati) ikipepea katika viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.

Msaada wa haraka wahitajika kwa wakimbizi nchini Sri Lanka baada ya mashambilizi -UNHCR

Wahamiaji na Wakimbizi

Takribani wiki tatu  baada ya kutokea mashambulizi  makubwa wakati wa sherehe  za pasaka nchini Sri Lanka, shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa limeelezea wasiwasi kuhusu madhara ambayo mashambulizi hayo yamesababisha kwa  wa Sri Lanka wenyewe, na kwa hali inayoendelea  kwa maelfu ya wakimbizi na waomba hifadhi waliokimbia makwao baada ya mashmbulizi hayo.

UNHCR inashikiana kwa karibu na serikali, Umoja wa Mataifa na washirika na jamii kuhakikisha kuwa wakimbizi wote na waomba hifadhi wako salama.

Tunaendelea kuwasaidia wale waliohama huku mazungumzo yakiendela na mamlaka kutambua makao mbadala hadi pale wakimbizi watakaparejea makwao. Tumepeleka wafanyakazi zaidi kusaidia serikali, msemaji wa UNHCR  Babar Baloch alisema.

Kwa sasa wakimbizi 1,060 na waomba hifadhi, wakiwemo wanawake na watoto wanaishi katika misikiti, vituo vya polisi na vituo vya kijamii wakihofia kuzuka ghasia na vitisho. Wengi waliikimbia nchi zao  kufuatia imani zao za dini au siasa.

UNHCR inatoa chakula, madawa na vifaa vya makao hukua ikajaribu kutambua mahitaji zaidi.

Kwa sasa kuna wakimbizi 1,700 waliosajiliwa na waomba hifadhi nchini Sri Lanka. Mamia bado wanaishi kwa amani kwenye vijiji vyao. Sri Lanka imetoa ulinzi kwa miaka mingi kwa wakimbizi kutoka dini na nchi tofauti.