Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO yatoa msaada ya dawa na vifaa vya dharura Gaza

Mratibu Maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye kwenye maeneo ya Plestina yanayokaliwa, Jamie McGoldrick, atembelea wagonjwa  katika hospitali ya Al-Shifa , Gaza akiwa pamoja na madaktari na wajumbe wa WHO.
UNRWA/Khalil Adwan
Mratibu Maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye kwenye maeneo ya Plestina yanayokaliwa, Jamie McGoldrick, atembelea wagonjwa katika hospitali ya Al-Shifa , Gaza akiwa pamoja na madaktari na wajumbe wa WHO.

WHO yatoa msaada ya dawa na vifaa vya dharura Gaza

Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Afya Duniani (WHO) hii leo limetoa msaada wa dawa na vifaa muhimu kwa badhi ya vituo vya huduma ya dharurua Gaza ili kukabiliana mahitaji ya kiafya katika ukanda wa Gaza .

Msaada huo ambao ni ukarimu wa nchi za muungano wa Ulaya  utawezesha vituo  10 vya  dharura vinavyoendeshwa na wizara ya afya ya Palestina kwa ushirikisano na shirika la hilali nyekundu, Kuweza kutoa huduma za afya hususan kwa majeruhi wa viungo katika maandamano.

Dr Gerald Rockenschaub,  ambaye ni mkuu wa ofisi ya WHO Palestina ameshukuru Muungano wa nchi za Ulaya kwa msaada katika Ukanda wa Gaza, akiongeza kuwa 
"Upungufu wa rasilimali  na huduma muhimu za afya kwa majeruhi wa viungo wa  muda mrefu unaweza  kusababisha ulemavu au hata matokeo mabaya ya kiafya”.

Aidha WHO na mashirika ya afya  wanafanya kazi pamoja ili kuhakikisha kuwa huduma za dharura TSPs zina uwezo wa kuboresha afya ya wagonjwa, kupunguza hatari ya matatizo ya kuzuia maumivu au kupoteza viungo, na kuhakikisha matokeo bora ya afya.

WHO imesema msaada huo  ni muhimu sana kutokana na  idadi kubwa ya  majeruhi yatokanayo na majeraha ya risasi za moto,  hiyvo inafanya jitihada kuimarisha ngazi zote za usimamizi wa majeraha na kuhakikisha kuwa kabla ya kufikishwa hospitali, timu za huduma za dharura  TSP zina dawa muhimu na vifaa vya matibabu ya awali kwa waliojeruhiwa.
Msaada huo utaweza kusaidia  mahitaji ya watu 120,000 wasio na majeraha ya kutisha  sana au wagonjwa 20,000 waliojeruhiwa vibaya. Mbali na dawa na vifaa vya matibabu, WHO imetoa mahema 4 kwa kila TSP ili kuhakikisha timu zina nafasi ya kutosha kutibu wagonjwa wenye shida tofauti. Vituo vitano vimepewa  jenereta zinazoendesha huduma za msingi, kama vile utoaji wa hewa ya oksijeni kwa wagonjwa.

WHO pia imetoa  mahema yanayoweza kutengenezwa ambayo yanaweza kusimamishwa ndani ya dakika chake wakati  wa dharura na pia yanayoweza  kuhamishwa haraka kwa maeneo mbadala ili kutibu watu wanaohitaji hudma za dharura.
Mbali na mahitaji makubwa yaliyotekelezwa, WHO imetoa wito wa dola milioni 5.3 wakati huu ambapo wanajiandaa na  maadhimisho ya mwaka mmoja  ya maandamo yajayo ambayo yanaweza kusababisha majeruhi zaidi.

WHO na washirika wa kikundi cha afya walitengeneza mpango wa dharura kushughulikia mahitaji ya afya ndani ya masaa 96 ili  kuzuia kifo na ulemavu. Ili kuongeza zaidi ngazi zote za utunzaji wa majeraha.