Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mchango wa wanawake katika amani ya kudumu Kenya ni dhahiri-Embrace

Ida Odinga kinara wa kikundi cha kusongesha harakati za kuleta amani kwa jina la Embrace na Rachel Shebesh katibu tawala kwenye wizara ya mambo ya nje Kenya.
UN News Kiswahili/ Grece Kaneiya
Ida Odinga kinara wa kikundi cha kusongesha harakati za kuleta amani kwa jina la Embrace na Rachel Shebesh katibu tawala kwenye wizara ya mambo ya nje Kenya.

Mchango wa wanawake katika amani ya kudumu Kenya ni dhahiri-Embrace

Wanawake

Mkutano wa 63 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW63 umeingia siku ya sita hii leo Jumatatu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambako kunafanyika mikutano kando ikiratibiwa na nchi wanachama ili kuonyesha kwa kina kile inachofanya mashinani kumnasua mwanamke.

Moja wa mikutano hiyo ya kando ni ule ulioangazia uongozi wa wanawake katika kuelekeza kujenga utamaduni wa amani kwa ajili ya jamii endelevu ukisimamiwa na Kenya na Indonesia chini ya uwezeshaji wa Umoja wa Mataifa.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, ili kuwepo amani ya kudumu, sauti za wanawake zinahitajika, kuanzia kuzuia, kusuluhisha mizozo na kuleta uwiano na kuimarisha uchumi baada ya mizozo na kwamba ushiriki wa wanawake kikamilifu unaimarisha fursa za makubaliano ya amani kudumu.

Ni kwa kuendana na dhamira hiyo ndipo wanawake wenye ushawishi nchini Kenya wamechukua jukumu la kuchagiza amani na kuanzisha kikundi cha kusongesha harakati za kuleta amani kwa jina la Embrace. 

Mmoja wa wanawake hao, Bi Ida Odinga ambaye ni mwenyekiti wa kundi hilo pindi tu baada ya mkutano wao amezungumza na Idhaa ya Kiswahili ambapo amesema

Sauti ya Ida

Kwa upande wake bi Rachel Shebesh katibu tawala kwenye wizara ya maswala ya jinsia, wazee na watoto Kenya na mwanachama wa Embrace amesema lengo na kundi hilo ni pamoja na

Sauti ya Shebesh