Msiba huu umetuathiri sana, marehemu ni marafiki na wafanyakazi wenzetu - Joyce Msuya
Wakati maombolezo ya vifo vya wafanyakazi 21 wa Umoja wa Mataifa yakiendelea katika ofisi mbalimbali duniani kote, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP, mjini Nairobi Kenya ni miongoni mwa mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopata pigo la ajali hiyo.
Akiongea na Idhaa ya kiswahili ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya simu kutoka Nairobi kenya kandoni mwa mkutano wa Baraza kuu la mazingira duniaambapo wengi wa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa walikuwa wakielekea , Joyce Msuya ambaye ni kaimu Mkurungezi wa UNEP amesema…….
Sauti ya Joyce Msuya
Na vipi msiba huu umeathiri maudhui ya mkutano huo wa siku 5 uliowakusanya wanamazingira kutoka pande zote za dunia ?
Sauti ya Joyce Msuya
Ameongeza kuwa Umoja wa Mataifa unaendelea kuwasiliana na ndugu na jamaa wa marehemu popote walipo ili kutoa msaada wa hali na mali , na pia kuandaa mchakato wa mazishi katika kuwaenzi marehemu.