Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makumi ya maelfu ya wakimbizi kutoka Nigeria wamiminika Cameroon-UNHCR

Kambi ya wakimbizi huko kaskazini mwa Cameroon ikihifadhi wakimbzi wa Nigeria. Boko Haram wamekuwa wakileta ghasia na kuua raia nchini Nigeria na nchi jirani.
OCHA/Ivo Brandau
Kambi ya wakimbizi huko kaskazini mwa Cameroon ikihifadhi wakimbzi wa Nigeria. Boko Haram wamekuwa wakileta ghasia na kuua raia nchini Nigeria na nchi jirani.

Makumi ya maelfu ya wakimbizi kutoka Nigeria wamiminika Cameroon-UNHCR

Amani na Usalama

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR nchini Cameroon, limesema linaendelea kupokea wakimbizi kutoka Nigeria ambao wanakimbilia  Cameroon kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara yanayofanywa na kundi la Boko Haram. UNHCR imesema baadhi yao ni wameshakimbia nchi  yao zaidi ya mara tano hadi kumi kwa sababu hawana njia nyingine zaidi ya kujinusuru ili kusaka usalama

Ni sauti za purukushani za wakimbizi walioko safarini kuelekea Cameroon wakitokea Nigeria, wakimbizi hawa wanaonekana na virago vyao, iwe kwenye mkokoteni au kichwani. Watoto, wanawake kwa wanaume wote lengo ni kusaka maeneo salama.

Wanakimbia machafuko kutoka eneo la Rann ilililoko kilometa saba kutoka kituo cha mpakani cha Cameroon. Mmoja wa wakimbizi hao kutoka Nigeria ni Kellou Maloum Modu.

(Sauti ya Modu)

“Wakati wanajeshi waliondoka, hatukuwa na namna nyingine isipokuwa kuondoka. Hatukuwa na chochote cha kujikinga kwa hiyo ilikuwa bora kuondoka.”

Naye Hebibi Toudjum aliwasili kutoka Rann na hakukosa simulizi ya walichoshuhudia.

(Sauti ya Hebibi)

“Boko Haram waliwaua watu wengi, tulifika hapa siku sita zilizopita.”

Kambi ya Gubio Maiduguri imepokea wakimbizi wapya 4500 tangu Novemba 2018, wengi wao katika wiki za karibuni kufuatia mashambulizi ya kundi lenye silaha la Baga, karibu na ufukwe wa ziwa Chad, Kaskazini Mashariki mwa Nigeria
OCHA/Leni Kinzili
Kambi ya Gubio Maiduguri imepokea wakimbizi wapya 4500 tangu Novemba 2018, wengi wao katika wiki za karibuni kufuatia mashambulizi ya kundi lenye silaha la Baga, karibu na ufukwe wa ziwa Chad, Kaskazini Mashariki mwa Nigeria

Wakimbizi wanawasili na kupokelewa na UNHCR ambayo inawapatia makazi katika kambi ya muda. Geert Van de Casteele ni mwakilishi wa shirika hilo nchini Cameroon.

(Sauti ya Casteele)

“Licha ya kwamba tuna changamoto nyingi, lakini tunawaleta watu zaidi na kwa sasa, wafanyakazi wenzangu wameweza kufanya mahesabu kwa muda mfupi ambapo katika kipindi cha miezi mitatu ijayo UNHCR itahitaji takriban kati ya dola milioni kumi na moja”.

Mwezi Januari mwaka huu wa 2019 Umoja wa Mataifa kwa ushirikiano na serikali ya Cameroon na wadau walitoa tangazo la mahitaji ya kibinadamu ambayo yanalenga nchi nzima, ikiwemo maeneo ambayo yameathiriwa na Boko Haram. Takriban watu milioni 4.3 kutoka Cameroon, wengi wakiwa ni wanawake na Watoto, wana mahitaji ya dharura.