Skip to main content

Kila mtu ana haki ya kufurahia utulivu wa kijamii na kimataifa

Watoto kutoka jamii ya wachache wa Yazid wakila cakula.
UNHCR/N. Colt
Watoto kutoka jamii ya wachache wa Yazid wakila cakula.

Kila mtu ana haki ya kufurahia utulivu wa kijamii na kimataifa

Haki za binadamu

Disemba 10, dunia itaadhimisha miaka sabini tangu kuridhiwa kwa tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa. Nyaraka hii imetajwa kuwa ya kipekee kwani imezingatia haki zote na imejumuisha makundi ya watu wote katika jamii ikiwemo makundi ya watu walio wachache. 

 

Tamko hilo lenye ibara 30 imegusa maeneo yote ya haki za wote na nchi nyingi zimechukua muongozo wake katika kutunga sheria za nchi zao.

Ibara ya 28 ya tamko hilo inasema kuwa kiila mtu ana haki ya kufurahia utulivu  wa kijamii na kimataifa ambapo haki zote zizlizopo kwenye tamko la haki za binadamu zinaweza kufurahiwa.

Ibara hii inaelezea umuhimu wa kuweka mazingira yanayowezesha mtu kufurahia haki zote kama zilizoorodheshwa katika tamko la haki za binadamu.