Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania iimarishe hatua kuepuka mgongano wa maslahi kwenye utendaji- CAG

Profesa Musa Juma Assad ambaye ni mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali nchini Tanzania, wakati wa mahojiano na Idhaa ya Kiswahili
UN News/Assumpta Massoi
Profesa Musa Juma Assad ambaye ni mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali nchini Tanzania, wakati wa mahojiano na Idhaa ya Kiswahili

Tanzania iimarishe hatua kuepuka mgongano wa maslahi kwenye utendaji- CAG

Masuala ya UM

Mkutano wa wajumbe wa jopo la wakaguzi wa nje wa Umoja wa Mataifa ukimalizika leo kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Tanzania ambayo ni mjumbe wa jopo hilo imesema imekuwa ni fursa ya kubadilishana mawazo hususan masuala ya kuepusha mgongano wa maslahi, udanganyifu na rushwa.

Katika mkutano huo, Tanzania inawakilisha na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Profesa Mussa Assad ambaye katika mahojiano maalum na Arnold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, amesema wamejifunza mengi hususan taratibu za kuepusha mgongano wa maslahi

Tanzania imeteuliwa kuwa mtazamaji wa bodi ya ukaguzi ya Umoja wa Mataifa sambamba na mjumbe wa jopo la wakaguzi wa nje, na hii ni baada ya kuwa mjumbe wa bodi ya  ukaguzi ya Umoja wa Mataifa kwa miaka sita, ujumbe ambao ulimalika mwezi Julai mwaka huu.