Mwanafamilia hapaswi kushinikizwa kujiunga au kutojiunga na kikundi - UDHR
Mwanafamilia hapaswi kushinikizwa kujiunga au kutojiunga na kikundi - UDHR
Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, #UDHR likitimiza miaka 70 mwezi disemba mwaka huu wa 2018, harakati mbalimbali zimekuwa zikifanyika ili kukumbusha binadamu haki zao za msingi zilizotajwa bayana ndani ya nyaraka hiyo yenye ibara 30.
Nchi zilizotia saini na kuridhia tamko hilo, zinakuwa ni sawa na kufunga pingu ya kwamba zitatekeleza haki hizo na la msingi ni kwamba haki hizi zinachukuliwa kwa umoja wake badala ya kuchagua moja na kuacha nyingine.
Miongoni mwa haki hizo ni ile ya kujiunga au kutojiungana kikundi chochote ambayo imeelezwa bayana katika ibara ya 20 ya tamko hilo. Katika mfululizo wetu wa uchambuzi wa ibara hizo leo mtaalamu wetu ni wakili Aloyce Komba kutoka Tanzania ambaye katika mahojiano na Arnold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anachambua ibara hiyo kwa kuanza na ainisho.