Tunalaani vikali shambulio dhidi ya ubalozi wa China Karachi
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali shambulio la jana Novemba 23 dhidi ya ubalozi wa China mjini Karachi nchini Pakistan. Shambulio hilo limekatili maisha ya maafisa wawili wa polisi wa Pakistan na raia wawili.
Pia wajumbe hao wa Baraza wamelaani shambulio lingine la kigaidi lililotokea kwenye soko la Khyber jimbo la Pakhtunkhwa Pakistan siku hiyo hiyo na kuua watu takriban 35 na kujeruhi wengine wengi
Wajumbe hao wameshukuru hatua za haraka zilizochukuliwa na uongozi wa Pakistan na kutoa pole kwa familia za wafiwa na kuwatakia nafuu ya haraka majeruhi.
Wajumbe wa Baraza wamerejea kusisitiza kwamba mikataba yote ya kimataifa kuhusu diplomasia ni lazima iheshimiwe na kutekelezwa. Aidha wajumbe wameyahimiza mataifa yote kufanya kila liwezekenalo kupambana na ugaidi wa aina zote lakini pia uchunguzi ufanyike na wahusika kuwajibishwa.