Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP inaomba Dola milioni 167 kusaidia wathirika wa ghasia CAR

Maafisa polisi kutoka ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini  Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wakiwa kwenye doria mjini Bouar nchini humo  katika picha hii ya Agosti 2018
MINUSCA/Hervé Serefio
Maafisa polisi kutoka ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wakiwa kwenye doria mjini Bouar nchini humo katika picha hii ya Agosti 2018

WFP inaomba Dola milioni 167 kusaidia wathirika wa ghasia CAR

Msaada wa Kibinadamu

Hali ya usalama   Jamhuri ya Afrika ya kati inazidikuwa tete ambapo leo shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP, limetoa wito wa  wito jumuiya za kikanda na jamii ya kimataifa kuchukua hatua haraka ili kuzuia kutokea janga la kibinadamu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini  mjini Geneva Uswisi msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP Herve Verhoosel amesema “ WFP ina wasiwasi na hali mbaya ya chakula katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na matukio ya hivi karibuni yanayofanya hali kuwa mbaya zaidi.”

Duru zinasema  wiki iliyopita kulitokea machafuko sehemu za Batangafo, kaskazini mwa nchi hiyo kati ya makundi yaliyojihami kwa silaha na kusababishakuchomwa kwa kambi ya wakimbizi wa ndani- IDP- na pia soko na nyumba za karibu na kambi hiyohali ambayo inawaongezea mateso watu wa eneo hilo ambao tayari  wanakabiliwa na uhaba wa chakula , makazi pamoja na mahitaji mengine muhimu.

WFP inasema taarifa za awali zinaonyesha kama watu kadhaa waliuawa na wengine kujeruhiwa na watu 27,000 hawana makazi huku 10,000 kati yaowamekimbilia msituni  

Kwa mujibu wa WFP,  hali katika maeneo mengine kama vile Bambari na Zemio ni ya wasiwasi  kutokana na kutokea kwa mapigano kati ya makundi yenye silaha kukabiliana na askari wa MINUSCA na kufanya hali kuwa mbaya zaidi.

Mbali ya hali hiyo WFP na washirika wake wanasema wataendelea na shughulika na utoaji wa misaada kwa wahjitaji lakini ili kukidhi mahitaji hayo takriban dola milioni 167 zinahitajika kuweza ili kukidhi mahitaji hayo kuanzia sasa hadi  mwisho wa mwaka wa 2019.