Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tunaomba dola 66 milioni ili kuhudumia wakimbizi wa Rohingya:WFP

Mkimbizi wa Rohingya, Tahara Begum, akiwa na mtoto wake katika kambi ya Kutupalong, Coxs Bazar, Bangladesh
UNHCR/David Azia
Mkimbizi wa Rohingya, Tahara Begum, akiwa na mtoto wake katika kambi ya Kutupalong, Coxs Bazar, Bangladesh

Tunaomba dola 66 milioni ili kuhudumia wakimbizi wa Rohingya:WFP

Msaada wa Kibinadamu

Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP linahitaji dola milioni 66 hadi mwezi Machi mwakani ili liweze kuendelea na usambazaji wa chakula kwa wakimbizi wa kabila la rohingya walioko ukimbizini nchini Bangladeshi.

Msemaji wa WFP mjini Geneva, Uswisi Herve Verhoosel   amewaambia waandishi habari hii leo kuwa fedha hizo zitaendeleza usambazaji wa mahitaji ambayo tayari wanawapatia wakimbizi hao kutoka Myanmar, akisema huko Cox Bazar peke yake wanatoa msaada wa chakula kwa zaidi ya wakimbizi 800,000 kila mwaka.

Bwana Verhoosel amezungumzia msaada wa dola milioni 22 kutoka Uingereza akisema.."Mchango mpya wa Uingereza wa dola milioni 22 utachangia katika shughuli mbalimbali za WFP. Hii ni pamoja na msaada wa chakula  kwa wakimbizi zaidi ya 680,000, vocha za ununuzi wa chakula kwa wakimbizi 250,000 pamoja na msaada muhimu wa lishe unaohitajika.”