Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ushirika wenu utaleta amani pembe ya Afrika:Guterres.

Meli katika bandari ya Djibout. Uhusiano mpya wa eneo hilo utaongeza harati katika bandari hiyo.
UN Photo/Evan Schneider
Meli katika bandari ya Djibout. Uhusiano mpya wa eneo hilo utaongeza harati katika bandari hiyo.

Ushirika wenu utaleta amani pembe ya Afrika:Guterres.

Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amepongeza uhusiano mpya ulioko sasa katika eneo la pembe ya Afrika akisema ni hatua moja muhimu katika kuleta amani kwenye eneo hilo.

Katika taarifa yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani, Katibu Mkuu amekaribisha  zaira ya mawaziri wa mashauri ya kigeni wa Eritrea, Ethiopia, na Somalia nchini Djibout kuungana na mwenzao wa Djibout, kuwa ni hatua nzuri ya kurejesha uhusiano baina ya mataifa hayo yaliyo katika   pembe ya Afrika.

Antonio Guterres amesema makubaliano yaliyofikiwa  kati ya  mawaziri hao wanne ya kushirikiana ilikurejesha amani na utulivu katika eneo hio ni mfano mzuri wa kuigwa na sehemu zingine.

Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake ikizungumzia ziara hiyo iliyofanyika wiki hii,  Guterres amesema Umoja wa Mataifa uko tayari kuunga mkono mataifa ya eneo la pembe ya Afrika  kuimarisha mazuri yaliyopatikana katika kipindi kifupi kilichopita.