Pongezi Mauritania kwa uchaguzi wa amani:Guterres
Amani na Usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa António Guterres, amewapongeza watu wa Mauritania na serikali yao kwa kufanya uchaguzi wa bunge, mikoa na manispaa kwa amani nchini humo
Uchaguzi huo uliofanyika tarehe mosi mwezi Septemba ulishuhudia ushiriki mkubwa wa vyama vya siasa na wannchi waliojitokeza kupiga kura..
Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Katibu Mkuu anahimiza vyama vyote kuendeleakukumbatia hali ya amani amani wakati na baada ya kutangazwa kwa matokeo. Pia amewasihi viongozi wa kisiasa na wagombea kutatua migogoro na tofauti zao kupitia mazungumzo na kwa mujibu wa sheria.