Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana wasanii wana silaha ya kuchagiza haki za binadamu katika jamii zao

Sanaa ikitumika kuonyesha madhila ya utumwa. Hapa ni kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika moja ya matukio ya kukumbuka siku ya kutokomeza utumwa. (Picha:: UN /Devra Berkowitz)

Vijana wasanii wana silaha ya kuchagiza haki za binadamu katika jamii zao

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Sanaa ni moja ya mbinu inayoweza kutumika katika jamii kufikisha ujumbe na kuchagiza kuhusu malengo ya maendeleo endelevu ikiwemo lengo la haki za binadamu, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. John Kibego na tarifa kamili

Kwa kutambua mchango wa taalumu ya sanaa , ofisi ya haki za binadamu nchini Tanzania kwa ushirikiano na kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC Dar es slaam wameendesha mafunzo kwa vijana wasanii wa aina mbalimbali ili kuwachagiza kutumia vipaji vyao kusongesha mbele ajenda ya haki za binadamu katika jamii zao.

Miongoni mwa washiriki ni Hussein Mlele mratibu na mkurugenzi wa shirika la Mulika Tanzania   linalohusika na kutoa mafunzo kwa jamii kupityia sanaa ikiwemo afya , elimu ya uraia na haki za binadamu. Anasema mafunzo hayo yamewafungua macho

(HUSSEIN  )

Na baada ya kuelima watachukua hatua gani?

(SAUTI YA HUSSEIN )

Hivi sasa Hussein amejumuika na vijana wengine kutoka sehemu mbalimbali duniani kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu na vijana WYFUNA unaoendelea mjini Geneva Uswis .