Fikra bunifu zinahitajika katika upatanishi wa migogo: Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonya kuwa vita vinazidi kuwamtihani mgumu, na kupendekeza juhudi za pamoja, ushirikiano na kuwajumulisha wanawake na vijana katika kuvipatia ufumbuzi..
Guterres ameyasema hayo leo, katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York , Marekani wakati wa kikao cha Baraza la usalama kilichojadili mchango wa upatanishikatika kuzuia migogoro. Katika hotuba yake amehimiza kuwa kuwepo na fikira bunifu katika suala la upatanishi ni lazima
“ Ni lazima tlifanye suala la kuzuia kuwa kipaumbele chetu. Na uzuaji huo unajumuisha piakuwekeza katika upatanishi , kuleta amani na ,maendeleo endelevu."
Mkuu huyo wa Umoja wa mataifa ametaka mashirika kujitolea kwa kutumia upatanishi kama chombno cha kuokoa na kuboresha maisha ya mamilioni ya watu.
Ameongeza kuwa ana imani inawezekana kushughulikia na kubadilisha mkondo wamigogoro iliyotamalaki sasa kwa hivyo
‘ Ni lazima tuwe jasiri na wabunifu katika kuleta pamoja mbinu na uwezo uliopo wa kusaidia upatanishi.”
Katibu Mkuu pia amesem idadi ya migogo, makundi yaliyojihami kwa silaha na makundi yenye dhamira za kisiasa ambavyo vinafadhiliwa na magenge ya uhalifu vimechanganyika.
Amesema inafaa kuwekeza katika suala la upatanishi na maridhiano kwa kujumisha wadau wote na kutumia nyenzo mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii.
Kikao hicho kimehudhuirwa pia na Askofu mkuu wa Cantebury, Justin Welby, kama mwanajopo la Katibu Mkuu la baraza la juu la ushauri kuhusu upatanishi.