Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sherehe za Eid zaleta ahueni kwa wananchi wa Afghanistan

Usitishwaji mapigano wa masharti umetangazwa nchini Afghanistan katika kipindi cha Eid.Na mjini Herat watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.
UNAMA/Fraidoon Poya
Usitishwaji mapigano wa masharti umetangazwa nchini Afghanistan katika kipindi cha Eid.Na mjini Herat watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.

Sherehe za Eid zaleta ahueni kwa wananchi wa Afghanistan

Amani na Usalama

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA umekaribisha  tangazo la serikali nchini humo la kusitisha mapigano bila masharti  yoyote kwa ajili ya sherehe za Eid El Haj, na hivyo umetoa wito kwa pande kinzani kwenye mzozo kutumia fursa hiyo kukomesha ghasia.

Taarifa ya UNAMA iliyotolewa leo mjini Kabul, imemnukuu Mwakilishi maalum  wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan, Tadamichi Yamamoto  akisema kuwa sitisho la mapigano ambalo limekubaliwa na pande zote litaleta matumaini ya kufanyika kwa mazungumzo kati ya makundi husika ili kupata suluhu ya kisiasa.

Ameongeza kuwa “ni muhimu kuchukua nafasi hii kuzungumzia hatua za kumaliza  mgogoro ili raia wote wa Afghanistan waweze kufurahia amani wanayotaka.”

Miezi iliyotangulia  usitishwaji wa mapigano umeokoa maisha mengi ya raia na hivyo kudhihirisha jinsi raia wa Afghanistan  wanataka mgogoro huo uishe.

Katika miezi sita ya mwanzo ya mwaka huu, raia 1,692 waliuawa katika mapigano kati ya serikali na wapiganaji wa Taliban, ikiwa ni idadi kubwa zaidi katika muongo mmoja.

Mwaka huu pekee zaidi ya shule 130 nchini Afghanistan zilishambuliwa na vituo viwili vya afya viliharibiwa kabisa.

Habari zinasema kama hiyo haitoshi, matukio ya kushambulia watoa huduma za misaada nayo yaliongezeka kwa asilimia 20, ambapo wafanyakazi 23 waliuawa, 37 walijeruhiwa na 74 walitekwa nyara