Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mazungumzo ya Yemen; serikali na upinzani watumiwa mwaliko

Mjumbe maalum wa UN kwa Yemen Martin Griffiths akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sana'a nchini humo hii leo.
OSESGY/Emmanuel Bargues
Mjumbe maalum wa UN kwa Yemen Martin Griffiths akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sana'a nchini humo hii leo.

Mazungumzo ya Yemen; serikali na upinzani watumiwa mwaliko

Amani na Usalama

Dalili za kupata suluhu ya mzozo wa Yemen zinaanza kuonekana kufuatia taarifa zinazothibitishwa kuwa Umoja wa Mataifa umewasilisha mwaliko wa  mazungumzo kati ya serikali ya Yemen na wanamgambo wa kihouthi tarehe 6 mwezi  ujao huko Geneva, Uswisi.

Tangazo hilo lililotolewa leo huko Geneva, Uswisi linakuja baada ya mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Yemen Martin Griffiths kutangaza tarehe hiyo mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mapema mwezi huu.

Mzozo wa Yemen umedumu kwa zaidi ya miaka 3 na kusababisha vifo, njaa na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya kijamii na  raia wengi kusaka ukimbizi ndani na nje ya nchi hiyo.

Mazungumzo haya ya amani yanasonga kufuatia juhudi za pamoja zilizoanzishwa miaka 2 iliyopita chini ya uongozi wa mfalme Sheikh Jaber al-Ahmad al-Sabah wa Kuwait ambaye alijenga msingi wa mazungumzo yanayoendelea hivi sasa .