Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana waliookolewa pangoni Thailand wapatiwa uraia

Sanamu la Buddha kandoni mwa mto wa Mekong katika mji wa Chiang Rai ambako Vijana 12 wacheza soka waliokolewa   hivi karibuni
UN News/Elizabeth Scaffidi
Sanamu la Buddha kandoni mwa mto wa Mekong katika mji wa Chiang Rai ambako Vijana 12 wacheza soka waliokolewa hivi karibuni

Vijana waliookolewa pangoni Thailand wapatiwa uraia

Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limekaribisha hii leo  uamuzi wa serikali ya Thailand  ya kuwapa uraia vijana watatu na kocha wao wa soka , ambao hivi karibuni waliokolewa kutoka pangoni huko Chiang Rai katika operesheni isiyo ya kawaida iliyoongozwa na jeshi la nchi hiyo.

Carol Batchelor ambaye ni Mshauri Maalum wa UNHCR juu ya masuala ya watu wasiokuwa na utaifa amesema, “kwa kuwapatia uraia wavulana hawa na kocha wao, Thailand imewapa fursa ya sio tu kukamilisha ndoto zao balipia  kufikia malengo kadri ya uwezo wao hapo baadaye  zaidi na kufikia uwezo.”

Ameongeza kuwa Thailand imewapa utambulisho rasmi ambao ni njia ya kufikia matarajio yao na kushiriki kikamilifu kama wanachama kamili katika  jamii zao.

Aidha Bi Batchelor  amesema kuwa watu  ambao hawatambuliki rasmi na taifa lolote  huchukuliwa  kama “wasio na utaifa “ na mara nyingi hujikuta bila haki wala huduma za msingi. 

Amesema watu hao hawawezi kusafiri, kuolewa, kumiliki mali au kuajiriwa katika jamii wanamoishi na kwamba mara nyingi matatizo yao  huwa hayapatiwi  ufumbuzi.

UNHCR inasema kuwa Thailand imekuwa mstari wa mbele  kikanda katika kuchukua hatua ya kukomesha hali ya watu kukosa utaifa ambapo watu wapatao 100,000 wamepatiwa uraia wa nchi hiyo  tangu mwaka 2008.

Halikadhalika serikali hiyo  imejitolea kutafuta ufumbuzi wa   kitaifa kwa watu 480,000 ambao hawana utaifa  ifikapo mwaka  2024.

Ni kwa mantiki hiyo UNHCR  na washirika  kupitia kampeni  ya “I belong” kwa Kiswahili “Mimi ni wa” itaendelea kutoa ushirikiano kwa  serikali ya Thailand katika kutokomeza hali ya kutokuwa na utaifa kwenye ukanda huo.