Kitendo cha Zambia kumrejesha kinguvu nyumbani mwanasiasa hakikubaliki-UNHCR
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR limesema lina wasiwasi mkubwa kuhusu taarifa za kurejeshwa nyumbani kinguvu kwa raia mmoja wa Zimbabwe aliyekuwa anasaka hifadhi Zambia.
UNHCR kupitia taarifa yake ya leo imetoa wito kwa Zambia ifanye uchunguzi wa haraka kuhusu tukio hilo.
Inaripotiwa kuwa hapo jana mwanasiasa mmoja mwandamizi wa Zimbabwe, ambaye hakutajwa jina, alifika mpakani mwa Zimbabwe na Zambia na kueleza nia yake ya kupewa hifadhi ya kisiasa nchini humo.
Hata hivyo maafisa wa Zambia hii leo wamemkabidhi kwa mamlaka za nchi yake licha ya mahakama ya Zambia kuamua vinginevyo.
UNHCR inasema kumrejesha nyumbani bila hiari mkimbizi yeyote au msaka hifadhi ni ukiukwaji mkubwa wa sheria ya kimataifa ya wakimbizi.