Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

CSW yaleta nuru kwa wamasai huko Arusha-Tanzania

Mtoto wa kimasai nchini akipata maarifa kupitia simu ya kiganjani .
Picha/Worldreader
Mtoto wa kimasai nchini akipata maarifa kupitia simu ya kiganjani .

CSW yaleta nuru kwa wamasai huko Arusha-Tanzania

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Mkutano wa 62 wa kamisheni  ya hali ya wanawake duniani, CSW uliofanyika mapema mwaka huu jijini New York, Marekani umezaa matunda kwa wanawake wa jamii yakimasai mkoani Arusha nchini Tanzania.

Akizungumza kwa njia ya simu na Idhaa ya kiswahili ya Umoja wa Mataifa, Alais Esoto ambaye ni mkurugenzi wa shirika la kiraia la Naserian linalojishughulisha na masuala ya haki na maendeleo  kwa  wanawake  na wasichana wa jamii ya wamasai  amesema baada ya kupata mafunzo ya kumkwamua mwanamke kwenye mkutano huo wameanzisha miradi mbalimbali ambayo imekuwa mkombozi kwa makundi hayo.

Sauti ya Alais Esoto

Pamoja na kuwekeza katika elimu ya watoto wa kimasai, bwana Esoto  amezungumzia  pia mradi wa ufugaji unaosaidia wanawake masikini.

Sauti ya Alais Esoto

Shirika hilo la kiraia la Naserian limekuwa likishirikiana na wadau mbalimbali katika kutokomeza mila mbalimbali ikiwemo ukeketaji wa wasichana na wanawake mkoani Arusha.