Kuoanisha SDGs ni muhimu katika kuyafanikisha-WWF
Ukuaji wa Kiuchumi
Utashi wa kisiasa ni msingi muhimu kwa nchi katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ifikapo mwaka 2030 hivyo ni muhimu kwa serikali kuweka mchakato wa kisiasa katika kuwezesha hilo.
Hiyo ni kwa mujibu wa Innocent Maloba kutoka shirika la World Wide Fund for Nature, WWF, linalofanya kazi katika takriban nchi 100 kote duniani akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.
Bwana Maloba amesema ni muhimu kwa nchi kuelewa kwamba malengo yote yanashabihiana na hivyo…
(Sauti ya Innocent Maloba)
Kwa mantiki hiyo amebainisha mambo ya kuzingatia
(Sauti ya Innocent Maloba)