Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IOM yatoa dola elfu 75 kusaidia waathirika wa mafuriko Lao

Kijiji cha kawaida nchini Lao.Ambako mvua kubwa zimesababisha kupasuka kwa kingo za bwawa la maji la kuzalisha umeme la  Xenamnoy huko  jimbo la Champassak
UNICEF/Rachel O'Brien
Kijiji cha kawaida nchini Lao.Ambako mvua kubwa zimesababisha kupasuka kwa kingo za bwawa la maji la kuzalisha umeme la Xenamnoy huko jimbo la Champassak

IOM yatoa dola elfu 75 kusaidia waathirika wa mafuriko Lao

Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM, limetoa dola elfu 75 kusaidia waathirika wa mafuriko yaliyosababishwa na kupasuka kwa kingo za bwawa la maji la kuzalisha umeme la  Xenamnoy huko  jimbo la Champassak kusini magharibi mwa jamhuri ya Kidemokrasia ya  watu wa Lao .

 

Kwa mujibu wa mamlaka za Lao, kupasuka kwa kingo hizo na mafuriko kulichochewa na mvua kali zitokanazo na  kimbunga Son-Tinh kilichokumba ukanda huo na kuathiri  zaidi ya majimbo 11 na zaidi ya watu 16,256 nchini humo.

Hali ni mbaya zaidi katika vijiji 13 vya wilaya ya Sanamxay, ambako watu 6,351 wameathirika.

IOM inasema watu 3,060 wamepoteza makazi na sasa wamehamishiwa katika makazi ya muda ya dharura.

 Mkuu wa IOM nchini Lao Misato Yuasa amesema mpaka sasa  watu 26 wameripotiwa kufariki dunia huku wengine 131 hawajulikani walipo na zaidi ya yote..

“ IOM sasa inatumia  ujuzi wake  wa kimataifa katika kubabiliana na  dharura katika kuisaidia  serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu Lao, kama  wanachama wapya zaidi ya yote  kukabiliana na hali ya janga hili kubwa. Lakini pia tumejitolea kuwasaidia watu hawa hapo baadaye mpaka tuhakikishe  maisha yao yanarejea na kwa kuwafikia  wafadhili wa kimataifa”.

IOM imewapeleka nchini Lao wataalamu wake wa kiufundi kwenye masuala ya ujenzi wa makazi ya dharura, usimamizi wa makazi, uhamiaji na masuala ya vifaa. Wataalamu hao wanatoka ofisi ya IOM ya kanda ya Asia-Pasifiki iliyoko Bangkok, Thailand.

Misaada ya  dharura ya uokoaji katika majanga inapangwa kwa sekta ambapo IOM inashirikiana na wataalam wengine kuoka  UN Habitat na Wizara ya Ujenzi wa Umma na Nyumba. Pia na  makundi ya   wataalamu wa afya na maji kutoka WHO na  huduma za maji na kujifasi au WASH kutoka UNICEF.

IOM, ilianza operesheni zake huko Lao mwaka 2002 na mwezi Juni mwaka 2018 nchi hiyo ilijiunga na shirika hilo ikiwa ni mwanachama wake wa 171.

 

Tags: IOM, LAO, UNHabitat, UNICEF