Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kujiadhari kabla ya shari ndio dawa mujarabu ya majanga: FAO

Ethiopia iliwahi kukumbwa na  ukame  uliosababisha mifgo wengi kufarikina mazao kunyauka hali iliyopelkea kuhitajimmsaada wa kibinadamu. FAO inasem aukijipanga mapema na kutoa msaada wa awali ukame hauleti hasara kubwa.
WFP/Melese Awoke
Ethiopia iliwahi kukumbwa na ukame uliosababisha mifgo wengi kufarikina mazao kunyauka hali iliyopelkea kuhitajimmsaada wa kibinadamu. FAO inasem aukijipanga mapema na kutoa msaada wa awali ukame hauleti hasara kubwa.

Kujiadhari kabla ya shari ndio dawa mujarabu ya majanga: FAO

Msaada wa Kibinadamu

Kuchukua tahadhari za mapema katika nchi zinazotabiriwa kukumbwa na majanga ya asili kunaweza kuzuia tishio la kutokea zahma ya kibinadamu  au kunaweza kudhibiti athari  kwa mujibu wa ripoti  mpya iliyotolewa leo na shirika la chakula na kilimo duniani , FAO.

Kwa mujibu wa shirika hilo ushahidi umedhihirisha kwamba tahadhari na hatua za mapema zilisaidia kupunguza athari za ukame wa mwaka 2017 ulioikumba Kenya, Somalia na Ethiopia.

Ushahidi mpya kuwa uingiliaji wa mapema ulipunguza athari za ukame wa mwaka 2017 katika eneo la pembe ya Afrika uko katika ripoti mpya.

Ripoti hiyo iliyotolewa leo mjini Roma Italia inasema kila dola moja iliyotumiwa na FAO kusaidia mifugo  mapema nchini Kenya, Somalia na Ethiopia mapema mwaka 2017 wakati wafugaji wakijiandaa na msimu mwingine mbaya wa ukame, kila familia  ilipata faida ya hadi  dola 9 kwa sababu mifugo waliokufa kutokana na njaa, ukame, au magonjwa walikua wachache na uzalishaji wa maziwa ulipanda  mara tatu zaidi.

 

Msichana akiswaga mbuzi nchini Somalia kwenye eneo ambalo  ukame umeshamiri, halikadhalika uhaba wa maji.
FAO/Simon Maina
Msichana akiswaga mbuzi nchini Somalia kwenye eneo ambalo ukame umeshamiri, halikadhalika uhaba wa maji.

Mkurugenzi wa kitengo cha dharura na mipango ya ukarabati wa FAO, Dominique Burgeon, amesema kuwekeza  katika mikakati ya mapema katika kukabili majanga sio tu ni kitendo cha kiutu na cha kutumia akili bali pia kinapunguza gharama. Ameongeza kuweza  kulinda maisha ya watu kabla janga halijatokea ina maanisha ni kujenga mnepo kwa siku za usoni na kupunguza shinikizo katika masuala ya rasilimali.

Amesisitiza kuwa kuchukua hatua mapema ni muhimu na inawezekana na pia ni suala la uwajibikaji, kwanu ushahidi unaonyesha kwamba “ jinsi tunavyochukua hatua mapema ndivyo uwezo wa jamii kukabili majanga unavyokuwa mkubwa..”

 

Image
Picha na UM
Mazao kupungua Ethiopia kufuatia ukame. Hali hiyo huathiri zaidi familia nyingi na maskini . Picha: UM

Mathalani ripoti imetolea mfano wa Kenya ikisema kwa wastani wanyama wengine wawili kwa kila mkulima aliyepata msaada waliweza kuokolewa ikilinganishwa na  wale ambao hawakupata msaada; kila mtoto aliyekuwa chini ya umri wa miaka  mitano aliweza kunywa  nusu lita ya maziwa kwa siku jambo ambalo ni sawa na robo ya virutubisho wanavyostahili kuvipata kwa siku na kuwapa watoto asilimia 65 ya protini wanazohitaji kwa siku.

FAO inasema mpango huo wa kuzisadia jamii kabla ya kutokea majanga ya asili ni wa umuhimu sana kwani huokoa masiha ya watu na mifugo yao na pia ni uwekezaji muhimu kwa maisha yao ya baade.