Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nalaani vikali shambulio la kigaidi Sweida, huku ni kupuuza uhai wa watu:Guterres

Mvulana huyu akipita maeneo yaliyoharibiwa kufuatia mashambulizi nchini Syria.
© UNICEF/UNI150195/Diffidenti
Mvulana huyu akipita maeneo yaliyoharibiwa kufuatia mashambulizi nchini Syria.

Nalaani vikali shambulio la kigaidi Sweida, huku ni kupuuza uhai wa watu:Guterres

Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea mjini Sweida Syria siku ya Jumatano.

Duru zinasema zaidi ya watu 100 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika milipuko kadhaa ya mabomu wakati wa shambulio hilo.

Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake Guterres amesema amesikitishwa na kughadhibishwa na shambulio hilo lililofanywa na kundi la kigaidi la ISIL ambalo limepuuza thamani ya uhai na maisha ya watu.

Katibu Mkuu ametuma salamu za rambirambi kwa familia za wahanga wa shambulio hilo na kuwatakia ahuweni ya haraka majeruhi.

Pia ametoa wito wa kuhakikisha wote waliohusika na ukatili huo wanawajibishwa kisheria.

TAGS: Sweida, Syria, ISIL, ugaidi, Antonio Guterres