Skip to main content

Zimbabwe ni lazima kuheshimu haki zabinadamu wakati wa uchaguzi:UN

Bendera ya Zimbabwe. (Picha:UN/Maktaba)

Zimbabwe ni lazima kuheshimu haki zabinadamu wakati wa uchaguzi:UN

Amani na Usalama

Uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe unakaribia na wito umetolewa leo kwa wadau wote serikali, vyama vya kisiasi na wafuasi wao kuhakikisha kuwauchaguzi huo unafanyika katika mazingira  ya amani, utulivu , kuzingatia haki za binadamu na utawala wa sheria.

Wito huo umetolewa mjini Geneva Uswisi na  na ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa ikisisitiza  kuruhusu maandamano na mikusanyiko ya amani. Kwa mujibu wa msemaji wa ofisi za haki za binadamu,OHCHR, Bi Liz Throssel, uchaguzi huo umepangwa kufanyika Julai 30 na na maandalizi yanaendelea vyema

 (SAUTI YA LIZ THROSSELL)

“Inaleta matumaini  kuona mikutano ya hadhara  na maandamano ya amani vinafanyika  mjini Harare pamoja na matamshi ya uangalifu ya  asasi za kiraia yenye matumaini mema. Kuwepo kwa  baadhi ya makundi ya haki za binadamu ya kimataifa,  mbali ya tume ya haki za binadamu ya Zimbabwe na tume ya jinsia ya Zimbabwe kufuatilia  mazingira ya haki za binadamu kuelekea  uchaguzi wa taifa ni ishara inayokaribishwa.”    

Hata  hivyo amesema wana wasiwasi na ripoti zinazodizi kusambaa kutoka mikoani ambapo  baadhi ya wapiga kura wanatishiwapamoja na watu kulazimishwa kwenda katika mikutano ya kampeini. Kana kwamba hiyo haitoshi

 (SAUTI YA LIZ THROSSELL)

 “Pia kumekuwa na matumizi mabaya ya lugha dhidi ya wagombea wa viti vya wanawake. Tunaomba wakuu na vyama vya kisiasa na wafuasi wao kuhakikisha kuwa  uchaguzi hauvurugwi na  visa kama hivyo ili raia wote wa Zimbabbwe waweze kushiriki bila uoga  katika  mchakato wa uchaguzi wa kuaminika.”   

Amekumbushia ahadi  ya Juni 26 ambapo vyama vya kisiasa, chini ya tume ya amani na maridhiano ya taifa  nchini humo vilitia saini makubaliano ya kudumisha amani wakati wa kampeini na uchaguzi. Huu ni uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia unafanyika Zimbabwe baara ya Rais muasisi wa Taifa hilo Robert Mugabe kushinikizwa kuachia ngazi mwishoni mwa mwaka jana.